Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF)
Alhaj Mussa Mbaruku kushoto
akimkabidhi viatu Mweka Hazina wa timu ya African Sports, Sad Juma kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya Ligi Daraja
la pili makabidhiano hayo
yalifanyika uwanja wa CCM Mkwakwani mjini Tanga.
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF)
Alhaj Mussa Mbaruku kushoto
akimkabidhi viatu Mweka Hazina wa timu ya African Sports,Sad Juma kwa ajili ya kujiandaa na
michuano ya Ligi Daraja la
pili makabidhiano hayo yalifanyika uwanja wa CCM mkwakwani mjini
Tanga
Mbunge wa Jimbo la Tanga (CUF)
Alhaj Mussa
Mbaruku akisalimiana na wachezaji wa timu ya Jang'ombe ya Zanzibar
ambao wameweka kambi mkoani Tanga wakati alipokwenda kukabidhi vifaa kwa
timu ya African Sports.

TIMU ya African Sports
“Wanakimanumanu”imepata msaada wa vifaa vya michezo kwa ajili ya
kujiandaa na michuano ya Ligi daraja la pili itakayoanza kutimua
vumbi.
Vifaa hivyo ambavyo ni seti ya viatu vilitolewa juzi na Mbunge wa
Jimbo la Tanga (CUF) Alhaj Mussa
Mbaruku katika halfa iliyofanyika kwenye viwanja wa CCM Mkwakwani
mjini Tanga
Akizungumza mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo,Mbunge Mussa
alisema
ameamua kutoa vifaa hivyo ili kuweza
kuihamasisha kufanya vizuri katika mashindano hayo na hatimaye kuweza
kurudi ilipotoka.
Alisema licha ya timu hiyo kushuka daraja hivi sasa wanapaswa
kujiimarisha na kucheza kwa umakini mkubwa ili kuweza kucheza michuano
ya ngazi za juu.
“Mimi ni Mbunge lakini pia ni mwana michezo hivyo nitahakikisha
nazisapoti timu za mkoa huu kwa lengo
la kurejea kwenye makali yao ya zamani kwani michezo ni ajira
“Alisema.
Nay kwa upande wake,Mweka Hazina wa timu hiyo,Sad Juma alimshukuru
mbunge huyo kwa kutoa vifaa hivyo
ambavyo vitasaidia timu hiyo kuondokana na uhaba uliokuwepo.
“Kama unavyojua sisi tulikuwa na uhaba wa vifaa vya michezo
hususani
viatu na nyenginevyo hivyo alichotupa
mbunge tunamshukuru lakini tutakuwa nawe bega kwa bega “Alisema.
Hata hivyo alisema hivi sasa wanaendelea na maandalizi kwa ajili ya
kujiwinda na mashindano hayo wakiwa
na kikosi imara ambacho kimedhamiria kupata
mafanikio.
Habari kwa hisani ya Blog ya
Kijamii ya Tanga Raha.
Comments
Post a Comment