RICHARD MWANGULUBE/BUKOBA Mkoa wa Kagera umefanikiwa kujenga viwanda 91 katka kipindi cha mwezi Disemba 2017 na Juni mwaka 2018 ambapo kati ya hivyo 38 ni Viwanda vidogo ambapo ka ujumla wake vimefanikiwa kutengeneza ajira kwa watu 672.
Ujenzi huo wa viwanda unatokana na mkakati wa ‘Mkoa huo wa kujenga
viwanda vipatavyo 100’ kwa mwaka mkakati ambao kitaifa uliozinduliwa
mjini Dodoma na Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali
za mitaa(TAMISEMI) Selemani Jafo Oktoba mwaka jana 2018.
Katibu Tawala wa Mkoa wa Kagera(RAS) Diwani Athumani aliieleza
alipozungumza na Gazeti la Tanzanite One Ofisini kwake mjini Bukoba
katika mahojiano maalumu kwamba Viwanda hivyo ni vya kuchakata nafaka na
mafuta ya alizeti, viwanda vya matofali,useremala,ushonaji nguo,
kukoboa kahawa pamoja na viwanda vya sabuni.
Diwani Athumani Alisema pamoja na viwanda vidogo vinavyoendelea kujengwa
lakini tayari kuna Viwanda vikubwa vitano alivyovitaja kuwa ni
Kiwanda cha KADERES Plc kilichopo wilaya ya Karagwe kilichoanza
uzalishaji mwezi juni mwaka huu 2018 kinachohusika na uchakataji wa
maharage kwa kuyachambua kuondoa mawe, kusafisha, kuyapanga katika
madaraja na kuyafungasha tayari kwenda kwenye masoko ya ndani na nje ya
nchi.
Athumani alitaja viwanda kingine kuwa cha usindikaji kahawa cha Amir
Hamza (T) Ltd ambacho kimejengwa katika wilaya ya Bukoba eneo la Kibuye
na Kiwanda cha maji ya kunywa cha Bunena Dev Co Ltd kilichopo katika
Manispaa ya Bukoba.
Viwanda vingine vilivyoko katika hatua ya mwisho ya ujenzi ni Mayawa
kilichoko katika Manispaa ya Bukoba ambacho kitazalisha maji ya
matunda,mvinyo na maji ya kunywa,Kiwanda cha usindikaji wa nyanya na
pilipili cha Victoria Edibles Limited kinacojengwa Bukoba Vijijini na
Kiwanda cha Vinywaji Vikali cha Ambiance (T) Distilleries Limited
kinachojengwa katika Manispaa ya Bukoba eneo la Miembeni.
Aidha Athumani alisema Wawekezaji watano wameonyesha nia ya kuwekeza
katika ujenzi wa viwanda vikubwa ambao ni Kampuni ya Gesap Agro Farming
Co Ltd ya Morogoro kwa kujenga kiwanda cha maziwa katika wilayani
Missenyi na Kampuni ya BenBuild Investment Limited iliyoanza ujenzi wa
Kiwanda cha Vigae eneo la Kihanga wilayani Karagwe. Wawekezaji wengine ni KADERES PLC anayetarajia kujenga kiwanda cha
kahawa wilayani Muleba,Sying Investment Company Limited ya nchini China
inayotarajia kujenga kiwanda cha nyama katika wilaya ya Missenyi na
Kampuni ya Ndyanga Co Limited ya Muleba kujenga kiwanda cha maji
wilayani Muleba. Viwanda vikubwa vya muda mrefu vilivyoko mkoani humo ni pamoja na cha sukari cha Kagera Sugar kilichobinafishwa mwaka 2001. Viwanda vya uchakataji samaki vya Kagera Fish Co Ltd kilichopo eneo la
Kemondo wilaya ya Bukoba na Supreme Perch Ltd kilichopo Nyamukazi wilaya
ya Bukoba. Kiwanda cha Chai Kagera kilichopo Maruku wilaya ya Bukoba
kilichobinafishwa na Serikali mwaka 2000 kutoka iliyokuwa Mamlaka ya
Chai Kagera. Vingine ni viwanda vya kahawa vya TANICA kilichopo Manispaa ya Bukoba
,BUCOP kilichopo katika wilaya ya Bukoba eneo la Custom kilichoanzishwa
mwaka 1935 na Kiwanda cha Olam (T) Ltd kilichopo katika wilaya ya
Missenyi eneo la Bunazi. "Mkoa wa Kagera wenye Halmashauri nane ambazo ni Biharamulo,Bukoba Vijijini,Manispaa ya Bukoba,Kyerwa,Karagwe,Missenyi,Muleba
na Ngara umefanikia kutekeleza maelekezo ya Rais Dakta John Pombe
Magufuli katika suala zima la ujenzi wa Viwanda kwa kila Mkoa"
.Alisisitiza Diwani Athumani.
Pia amevitaja Viwanda vingine kuwa ni Kiwanda cha chai Kagera (Kagera
Tea Co.Ltd ambacho kipo eneo la Maruku Wilaya ya Bukoba ambacho
kilibinafisishwa na Serikali mwaka 2000 na kukabidhiwa kwa mwekezaji
ambaye ni mzawa.
Pia kuna Kiwanda cha TANICA ambacho kipo katika Manispaa ya Bukoba na
ambacho kilibinafisishwa na Serikali na kukabidhiwa Chama cha
Ushirika cha Mkoa (KCU 1990). Ameeleza Diwani Athumani.
Alifafanua kwamba Mkoa wa Kagera bado unazo fursa nyingi na muhimu kwa
ajili ya kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ambao unaweza
kufanywa katika sekta za Kilimo,Viwanda, Utalii, Uvuvi, Ufugaji ambapo
Mkoa tayari umetenga zaidi ya hekta 58,000. Hata hivyo alitaja baadhi ya changamoto zilizopo katika fursa za
uwekezaji kuwa maeneo mengi ya uwekezaji na ujenzi wa Viwanda
hayajapimwa, urasimu na mlolongo mrefu na ukiritimba katika upimaji wa
ardhi na kukosekana kwa mfumo mzuri na wa haraka katika upimaji wa
ardhi ilikuvutia zaidi wawekezaji Pia Changamoto nyingine ni upungufu wa watumishi katika halmashauri
za Wilaya za Mkoa huo alieleza Diwani Athumani Katibu Tawalawa Mkoa
huo wa Kagera.
Comments
Post a Comment