wheelchair access ramp design web city cpanel all on 6 price mantenimiento de cómputo sabong international live stream पैसा कमाने वाला गेम 娛樂城體驗金500 https://firelaila.com/ ทรูบิวตี้ พากย์ไทย 欧博官网手机版 rehvid new casinos online how can i add my website in google search engine オンラインカジノ online casino Online-Kasino ver 21 black jack online vegas joker online casino best online no deposit casinos bingo cayri online casino
MWANDISHI AANIKA SIRI NZITO ZA MAUAJI YA ALBINO KWENYE KITABU Posted by Unknown on September 14, 2017 KITAIFA
GEREZA LA KWITANGA KUWA KITUO KIKUU CHA MICHIKICHI-MAJALIWA Posted by Maendeleo Vijijini on July 29, 2018 Get link Facebook X Pinterest Email Other Apps Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama mazao ya michikichi yaliyokuwa yakikamuliwa kuwa mafuta ya kula wakati alipotembelea Gereza la Kwitanga mkoani Kigoma kujionea kilimo cha michikichi na uzalishaji wa mafuta ya mawese katika gereza hilo Julai 29, 2018. Kushoto ni Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojiwa na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, Kulia ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mhandisi Hamadi Masauni na kulia kwa Waziri Mkuu ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Peter Serukamba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imeliteua Gereza la Kwitanga lililopo wilayani Kigoma kuwa kituo kikuu cha uzalishaji wa zao la michikichi nchini. Hivyo ameuagiza uongozi wa gereza hilo waongeze nguvu katika uzalishaji wa michikichi kwa kupanua mashamba na kuongeza askari wenye ujuzi wa kilimo cha michikichi na kupanda miche mipya ya michikichi na kukata ya zamani. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumapili, Julai 29, 2018) wakati alipotembelea gereza hilo akiwa katika siku ya pili ya ziara yake ya kikazi yenye lengo la kufufua zao la michikichi mkoani Kigoma. Amesema Serikali imedhamiria kwa dhati kufufua kilimo cha zao la michikichi mkoani Kigoma, hivyo kila mwananchi lazima awe na shamba la michikichi.Katia hatua nyingine, Waziri Mkuu ameuagiza Mkuu wa Magereza Mkoa wa Kigoma Bw. Sabas Matolo kuhakikisha Gereza la Kwitanga linawezeshwa kwa kuwa na zana bora na za kisasa za kilimo yakiwemo matrekta na vifaa vya kuvunia ili waweze kuongeza uzalishaji wa mafuta. Pia, Waziri Mkuu amemuagiza Bw. Matolo awahamishe askari ambao ni wataalamu wa kilimo wenye ujuzi wa zao la michikichi kutoka kwenye Magereza mengine mkoani Kigoma na kuwahamishia katika gereza la Kwitanga ili kuimarisha uzalishaji. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua kitalu cha kuzalisha miche ya Michikichi cha Asasi ya Seed Change katika kijiji cha Simbo kwenye jimbo la Kigoma Vijijini Julai 29, 2018. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi hiyo, Alex Chetkovic. Wananchi wa Kijiji cha Kazuramimba wilayani Uvinza wakimshangilia Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati aliposimama kijijini hapa kuwasalimia Julai 29, 2018. Alikuwa njiani kwenda Uvinza kuendelea na ziara ya mkoa wa Kigoma. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa kijiji cha Kazuramimba wilayani Uvinza alipokuwa safarini kwenda Uvinza akiwa katika ziara ya mkoa wa Kigoma Julai 29, 2018. Comments
Comments
Post a Comment