- Get link
- X
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- X
- Other Apps
Geofrey Kikoti, Msimamizi wa Kiwanda cha Maji cha Rocks, akiwaonyesha waandishi baadhi ya mitambo inayotumika katika uzalishaji.
Na Mwandishi Wetu, Iringa
KIWANDA cha Maji cha Rocks kilichoko katika Kijiji cha
Iyayi, wilayani Kilolo kinatarajia kuongeza uzalishaji baada ya kuwasili kwa
mashine kubwa kuliko ya sasa.
Geoffrey Kikoti, msimamizi mkuu wa kiwanda hicho, alisema
kwamba, kwa sasa uzalishaji ni mdogo kutokana na uwezo wa mashine iliyopo.
“Uzalishaji wetu siyo mkubwa kwa sababu mashine iliyopo ni
ndogo, lakini tumepata mashine kubwa ambayo itaweza kuzalisha kiwango kikubwa
tofauti na sasa,” alisema Kikoti.
Kufungwa kwa mtambo huo mkubwa kutakuwa fursa nzuri kwa
wananchi wa maeneo hayo na Kata nzima ya Image, kwani watapatiwa ajira na hivyo
kujikwamua na hali ngumu ya uchumi.
Hata hivyo, Kikoti alisema kwamba, changamoto kubwa
inayowakabili kwa sasa ni masoko, ingawa wameanza mkakati wa kutafuta masoko
katika mikoa mingine nchini.
Kiwanda hicho kilichoanzishwa miaka mitatu iliyopita na
kuanza kazi mwaka 2011, ni cha pili kinachozalisha maji mkoani Iringa baada ya
kile cha Tanzathai kinachozalisha Maji Africa, ambacho kilikuwa cha kwanza
kuanzishwa nchini tangu mwanzoni mwa miaka ya 1990.
Kikwazo kingine ni ukosefu wa umeme wa uhakika, kwani
wanatumia jenereta ambalo gharama zake ni kubwa zaidi kuliko umeme wa gridi ya
Taifa, hali ambayo pia inaathiri uzalishaji.
“Kwa sasa tunazalisha lita 540 tu kwa wiki, lakini tukipata
umeme wa uhakika pamoja na kufunga mashine kubwa, tutakuwa na uwezo wa
kuzalisha mara tatu au nne zaidi,” alisema.
Comments
Post a Comment