NISHATI ya umeme
imeelezwa kuwa ni kiungo muhimu katika kuchochea uwekezaji wa viwanda hapa nchini ambao
utasaidia kuinua kwa kasi
uchumi ikiwemo maendeleo kwa watanzania.
Hayo yalibainishwa na Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Umeme
Tanzania (Tanesco) Dkt Tito
Mwinuka hivi karibuni wakati akizungumza katika baraza kuu la 47 la wafanyakazi wa Tanesco
mjini hapa ambapo alisema kwa
kutambua umuhimu huo wataihakikishia serikali malengo yao ya
viwanda
yanatimia.
Alisema kutokana na hali hiyo wataendelea kuhakikisha umeme wa
uhakika unapatikana katika
maeneo mbalimbali hapa nchini bila kuwepo kwa vikwazo vya namna yoyote ile ili azma hiyo
iweza kutimia kwa vitendo na
hivyo kuchochea kasi ya uchumi.
“Kama mnavyojua serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi
nchi kufikia ule wa kati wa
viwanda hivyo kufikia azma hiyo nishati ya umeme ni kiungo muhimu katika kuchochea
uwekezaji wa viwanda ambao
utasaidia harakati za maendeleo “Alisema
“Hivyo napenda kuihakikishia serikali kwamba tunatambua wajibu
tulio nao katika kutimiza
malengo hayo kwa kuongeza uwajibikaji na ufanisi kazini ambao ndio utakuwa dira ya kufikia
mafanikio “Alisema.
Kaimu Mkurugenzi huyo alisema tokea kuanzishwa kwa baraza
hilo limekuwa ni sehemu muhimu
kwa ajili ya kujadili mambo mbalimbali kwa maslahi ya wafanyakazi ambao wamewaamini
kuwawakilisha.
“Baraza hili limesaidia shirika kujua changamoto na
kero
zinazowakabili mahala pa kazi na kwa pamoja ufumbuzi wake
na
changamoto hizo zimepatiwa ufumbuzi kwa faida ya wafanyakazi
na shirika kwa ujumla
“Alisema.
Alisema serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi nchi
kufikia ule wa kati wa viwanda
hivyo ili kufikia azma hiyo nishati ya umeme nikiungo muhimu katika kuchochea uwekezaji wa
viwanda ambao utasaidia
harakati za maendeleo. Habari kwa Hisani ya Blog ya
Kijamii ya Tanga Raha.
Comments
Post a Comment