- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
WAKATI Yanga imetangaza rasmi kuwarejesha viungo wake, Deus
Kaseke na Mrisho Ngassa, wachezaji Kelvin Yondan na Hassan Ramadhan Kessy wamegoma kushinikiza kusaini mikataba mipya.
Yanga imewaongeza Ngassa na Kaseke ili kuimarisha kikosi
chake kuelekea mechi zilizosalia za Kundi D kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Majina ya wachezaji hao yametumwa kwenye Shirikisho la Soka
Afrika (CAF) pamoja na jina la mshambuliaji Heritier Makambo kutoka DC Motema
Pembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Jerry Tegete.
Ngassa na Kaseke wanafanya idadi ya wachezaji wapya
waliosajiliwa rasmi Yanga kufika wanne, baada ya viungo wengine, Feisal Salum
kutoka JKU ya Zanzibar na Jaffar Mohammed kutoka Maji Maji ya Songea iliyoshuka
daraja.
Uongozi wa Yanga unakabiliwa na mtihani juu ya wachezaji
waliogoma, kipa Benno Kakolanya, mabeki Juma Abdul, Andrew Vincent ‘Dante’,
Hassan Kessy na Kelvin Yondan ambao wamemaliza mikataba.
Wachezaji wote hao wamesusa mazoezi wakishinikiza kupewa
mikataba mipya na angalau Kakolanya, Abdul na Dante walifanya mazoezi kwa siku
kadhaa kabla ya kuungana na Kessy na Yondan kususa kabisa kufuatia kuona
viongozi hawatimizi ahadi.
Yanga inatarajiwa kuteremka uwanjani Jumatano Julai 18, 2018
mjini Nairobi, Kenya kumenyana na wenyeji, Gor Mahia katika mchezo wa Kundi D
Kombe la Shirikisho Afrika, kabla ya timu hizo kurudi Dar es Salaam kwa
marudiano Julai 29.
Yanga haijashinda mechi hata moja kati ya mbili za awali za
Kundi D baada ya kufungwa 4-0 na USM Alger nchini Algeria Mei 6 na kutoa sare
ya 0-0 na Rayon Sports ya Rwanda mjini Dar es Salaam Mei 16.
Yanga itacheza tena nyumbani, Uwanja wa Taifa ikiwakaribisha
USM Alger Agosti 19 kabla ya kwenda kukamilisha mechi zake za kundi hilo kwa
kumenyana na wenyeji, Rayon Sport Agosti 28.
Timu mbili za juu katika kundi hilo zitaungana na washindi
sita wa makundi mengine manne kwa mechi za nyumbani na ugenini za Robo Fainali
na zitakazofuzu zitasonga mbele, Nusu Fainali na baadaye Fainali.
Bingwa wa Kombe la Shirikisho atapata zawadi ya Dola za
Kimarekani, 1,250,000, mshindi wa pili dola 432,000 wakati timu zitakazoshika
nafasi za pili kwenye kila kundi zitapata dola 239,000 kila moja, nafasi ya
tatu dola 239,000 na za nne dola 150,000.
Comments
Post a Comment