- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU
WATOTO wachanga wanaopewa vyakula vigumu na maziwa ya mama
kuanzia umri wa miezi mitatu wanalala vizuri kuliko wale wanaopewa maziwa ya
mama pekee, tafiti mpya zinaweka wazi.
Ni rasmi kuwa yapasa kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa
kipindi cha miezi sita mfululizo. Wataalam wanasema wanawake wanatakiwa kufuata
ushauri huo, ingawa upo katika mapitio.
Katika utafti mpya, wataalam wa watoto (JAMA) wanasema kumpa
mtoto chakula kigumu kuna faida kwa mama na mtoto.
Watoto waliokuwa na matatizo machache ya kulala na akina
mama waliripotiwa kuboresha ubora wa maisha.
Na utafiti uliofanywa na vyuo vya Kings na St George huko
London ulichunguza watoto wa miezi mitatu 1,303 na waligawanywa katika makundi
mawili.
Kundi la kwanza walipewa maziwa ya mama pekee kwa muda wa
miezi sita, na kundi la pili walipewa vyakula vigumu na maziwa ya mama kuanzia
walipofikia umri wa miezi mitatu.
Wakati tafiti zikiendelea, wazazi walijaza fomu za kujibu
maswali kupitia mtandao kila mwezi mpaka watoto wao walipofikisha umri wa miezi
12, na baadaye walijaza kila baada ya miezi mitatu mpaka watoto walipofikisha
umri wa miaka mitatu.
Utafiti ulionyesha kwamba, watoto wachanga waliopo katika
kundi ambalo wanakula vyakula vigumu na maziwa ya mama walilala zaidi, waliamka
mara chache na walikuwa na matatizo machache ya usingizi kuliko wale waliopewa
maziwa ya mama pekee.
Akina mama wanaojua sana:
Mashirika ya NHS na WHO hivi karibuni yaliwashauri akinamama
kusubiri mpaka miezi sita kuwapa watoto wachanga vyakula vigumu, lakini
maelekezo haya kwa sasa yanapitiwa upya.
Licha ya kutolewa kwa ushauri huo rasmi, asilimia 75 ya
akinamama wa Uingereza wanawaanzishia watoto wachanga vyakula vigumu kabla ya
kufikisha miezi mitano, huku robo yake, yaani asilimia 26, wakisema kitendo cha
watoto kuamka usiku ndiyo sababu ya maamuzi yao, kwa mujibu wa utafiti wa
kuwalisha watoto wachanga mwaka 2010.
Profesa Gideon Lack kutoka Chuo cha Kings, London, alisema:
"Matokeo ya utafiti huu yanaunga mkono mtazamo wa wazazi kwamba
kutanguliza mapema vyakula vigumu kwa watoto wachanga kunaboresha usingizi.
"Wakati mwongozo rasmi wa awali unasema kuanzisha
vyakula vigumu mapema kwa watoto wachanga hakuwezi kuwafanya watoto walale
usiku mzima, utafiti huu mpya unapendekeza kwamba ushauri huo unatakiwa
kuchunguzwa upya kupitia uthibitisho mpya uliopatikana."
Kwa kiasi kikubwa, kundi la watoto waliopewa vyakula vigumu
mapema, waliripoti nusu ya kiwango cha aina ya matatizo makubwa ya kulala, kama
vile kulia na kukasirika haraka, hali ambayo inakosesha wazazi uwezekano wa
kupata muda wa kulala.
Akijibu utafiti huo, Prof. Mary Fewtrell, mtaalam wa lishe
katika Chuo cha Royal kinachohusiana na afya ya watoto, alidokeza kwamba
muongozo wa ulishaji wa watoto wachanga kwa sasa unaangaziwa upya.
Alisema, haya ni matokeo ya kuvutia kutoka kwa kundi kubwa
la watu tofauti lililo jaribiwa.
"RCPCH, tunapendekeza kwamba akina mama wanapaswa
kusaidiwa kunyonyesha watoto wao maziwa ya mama pekee kwa ajili ya afya kwa
kipindi cha miezi sita, na vyakula vigumu visianzishwe kabla mtoto hajafikia
miezi minne.
"Hata hivyo, ushahidi wa msingi unaotokana na ushauri
unaotumika sasa juu ya unyonyeshaji ni wa zaidi ya miaka 10, na kwa sasa una
hakikiwa huko nchini Uingereza na kamati ya ushauri wa kisayansi ya lishe.
"Tunatarajia kuona mapendekezo yaliyosasaishwa juu ya ulishaji wa mtoto
mchanga katika siku zijazo si mbali sana."
Chakula kipi
unachopaswa kumpa mtoto wako?
Vyakula vya awali vinaweza kujumuisha chakula kilichopondwa
au matunda laini na mboga mboga zilizopikwa - kama vile viazi, viazi vitamu,
karoti au tufaha.
Matunda laini kama vile matikiti au mchele wa watoto au
nafaka mchanganyiko pamoja na maziwa ya kawaida ya mtoto wako.
Watoto wengine wanapenda kuanza na vyakula vilivyo pondwa.
Watoto wengine wanahitaji muda zaidi ili waweze kuzoea hivyo wanapendelea
vyakula laini kabisa au vilivyo sagwa kwa mara ya kwanza.
Endelea kumpa vyakula mbali mbali. Inaweza chukua majaribio
mengi kabla mtoto wako hajakubali chakula kipya.
Kufikiria chakula cha kuwapa watoto wachanga katika miezi
sita ya awali inaweza kuwa utata, na akina mama wengi huwa na hofu kwamba
wanashutumiwa kwa kushindwa kuwanyonyesha vizuri watoto wao, na hujiona na
hatia wanapoanzishiwa watoto maziwa ya kopo au vyakula vigumu.
Mwezi uliopita chuo cha wakunga cha Royal, kilijibu juu ya
shinikizo wanalopata akinamama wapya kwa kutoa hadharani mwongozo mpya kwa
wakunga kuheshimu uchaguzi wa mwanamke kutonyonyesha.
Utafiti huu wa vitu vigumu sehemu ya ufadhili wake ulitoka
kwa shirika la viwango vya chakula, ambalo pia lilikuwa linachunguza namna gani
mzio (allergy) unatokea kwa watoto.
Msemaji wa FSA alisema: "Tunawahimiza wanawake wote kujikita
kwenye ushauri uliopo wa kunyonyesha maziwa ya mama pekee kwa miezi sita ya
kwanza.
"Kama kutakuwa na shaka yoyote kuhusu kile kilicho bora
kwa mtoto wako, tafadhali tafuta ushauri kutoka kwa daktari wako au mtaalamu wa
afya."
BBC
Comments
Post a Comment