- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
KAMATI ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF)
imebadili kupitisha mfumo wa Ligi Kuu na Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara
juu ya timu za kushuka na kupanda.
Na kuanzia msimu ujao FDL itachezwa katika makundi mawili
yenye timu 12 na timu 1 kutoka kila kundi itapanda kwenda Ligi Kuu wakati timu
zitakazoshika nafasi ya pili na ya tatu katika makundi yote zitacheza mtoano
kwa mechi za nyumbani na ugenini.
Taarifa ya TFF imesema kwamba washindi katika mechi hizo
watacheza na timu zilizoshika nafasi ya 17 na 18 katika Ligi Kuu kupata timu
mbili zitakazocheza Ligi Kuu, huku timu mbili za nafasi ya 19 na 20 zikishuka
daraja.
Timu hizo mbili za Ligi Kuu zilizoshika nafasi ya 17 na 18
kama zitapoteza michezo yao zitashuka Daraja kuungana na zilizoshika nafasi ya
19 na 20 na TFF imesema kwamba inafanya hivyo ili kuongeza ushindani wa Ligi
Kuu, FDL na SDL.
Comments
Post a Comment