- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Rachel Chengula akikabidhi mfano wa hundi ya Tsh. 125 Milioni kwa wawakilishi wa kituo cha Tumaini la Maisha kilichopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Fedha hizo zitatumika kugharamia matibabu ya watoto wenye saratani.
Taasisi ya Mo
Dewji imetoa msaada wa Tsh. 125 Milioni kwa kituo cha Tumaini la Maisha
kilichopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, ili kusaida kugharamia matibabu
ya magonjwa ya saratani kwa watoto wanaopatiwa huduma katika kituo hicho.
Akizungumza
katika hafla ya kukabidhi msaada huo iliyofanyika katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili, Meneja Miradi wa Taasisi ya Mo Dewji, Rachel Chengula alisema msaada
huo ni mwendelezo wa misaada ambayo imekuwa ikitolewa na taasisi kwa kituo
hicho.
Alisema
wanatambua hali ngumu ambayo wanapitia watoto hao wanapouguza magonjwa ya
saratani, hivyo wanaamini msaada huo utasaidia kuboresha huduma kwa watoto
waliopo kituoni hapo na kuwezesha watoto waliopo mikoani kusafirishwa ili
kufikishwa hospitalini na wao wapatiwe matibabu.
“Kama upo hai na
mwanao anapumua, mshukuru Mungu kuwa ana makusudi na wewe na ana makusudi na
mtoto wako. Usikatishwe tamaa na magonjwa, tunaamini kwamba watoto hawa
watapona na kurudi nyumbani, watasoma na watalitumikia Taifa letu,
“Kama
mnavyofahamu Mohammed Dewji amekuwa akifanya kazi na Tumaini la Maisha tangu
mwaka 2012 ili kusaidia watoto kupatiwa matibabu, na kupitia taasisi yake
tutaendelea kushirikiana ili kusaidia watoto wetu wapatiwe matibabu,” alisema
Chengula.
Nae Meneja wa
Wafadhili wa kituo cha Tumaini la Maisha, Alex Kaijage aliishukuru Taasisi ya
Mo Dewji kwa msaada ambao wamekuwa wakiwapatia na kuwaomba kuendelea kuwa na
moyo huo wa kusaidia matibabu ya watoto wenye saratani ili warejee katika hali
ya kawaida na kuendelea na shughuli zingine ikiwepo kusoma.
“Tunajua kwamba
tunahitaji sana sana hizi fedha kufanikisha matibabu ya hawa watoto, sio tu
usafiri wa kutoka huko wanakotoka na kuja bali hata dawa ambazo tunazipata kwa
sababu ya huu mchango ambao Mohammed Dewji ametuwezesha. Kwa sababu yenu watoto
hawa wanapata matibabu, kwa sababu yenu wanapona kwahiyo tunawashukuru sana,”
alisema Kaijage.
Kwa upande wa
mmoja wa wazazi ambao mtoto wake anapatiwa matibabu katika hicho, Hamisi
Samweli aliwataka wadau wengine wenye uwezo wa kifedha kuwa na moyo wa kusaidia
kama anavyofanya Mohammed Dewji ili watoto ambao wazazi wao hawana uwezo wa
kifedha wapatiwe matibabu.
Meneja
wa Wafadhili wa kituo cha Tumaini la Maisha, Alex Kaijage akitoa neon la
shukrani baada ya kupokea msaada wa Tsh. 125 Milioni kutoka kwa Taasisi ya Mo
Dewji ambazo zitatumika kugharamia matibabu ya watoto wenye saratani.
Baadhi
ya watoto ambao wanapatiwa matibabu katika kituo cha Tumaini la Maisha
kilichopo katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Comments
Post a Comment