- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU, DAR ES SALAAM
ALIYEKUWA kocha wa timu ya taifa ya vijana chini ua umri wa
miaka 17, Oscar Milambo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi mpya wa Ufundi wa Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF).
Uteuzi huo umefanywa na Kamati ya Utendaji ya TFF, baada ya
kumhamishia Salum Madadi aliyekuwa Mkurugenzi wa Ufundi katika nafasi ya
Mkurugenzi wa Mashindano.
Uamuzi huo umetolewa sambamba na maamuzi ya kumthibitisha
Kidao Wilfred kuwa Katibu Mkuu wa TFF katika kikao kilichofanyika Julai 12,
mwaka huu makao makuu ya TFF Karume, Ilala mjini Dar es Salaam.
Rais wa TFF, Wallace Karia, aliwasilisha suala la Kidao
kwenye kikao hicho na wajumbe kulipitisha na kuthibitisha rasmi Kidao katika
nafasi hiyo.
“Kamati ya utendaji pia imemthibitisha Salum Madadi kuwa
Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF. Nafasi ya Madadi aliyekuwa Mkurugenzi wa
Ufundi iliyobaki wazi kamati ya utendaji imemthibitisha Kocha Oscar Mirambo
kukaimu,” imesema taarifa ya TFF.
Katika hatua nyingine kikao hicho cha kamati ya Utendaji
kimemuondoa Clement Sanga aliyekuwa mwenyekiti wa Bodi ya Ligi (TPLB) kwenye
nafasi hiyo kwa kukosa sifa baada ya klabu ya Yanga kuwasilisha barua iliyokuwa
na maelezo ya kwamba Yusuph Manji ndio mwenyekiti wa klabu hiyo.
Kamati ya Uchaguzi imeelekezwa kuandaa uchaguzi wa kuziba
nafasi hiyo kamati ya utendaji imekubaliana kamati ya uchaguzi kuelezea
mchakato mzima wa uchaguzi ulivyokuwa wakati Sanga anaingia Bodi ya Ligi.
Comments
Post a Comment