- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Ndizi ya Madagasca: Je ndizi hii inaweza
kuokoa ndizi inayotumika duniani?
ANTANANARIVO, MADAGASCAR
NDIZI zinazomea porini ambazo huenda ndio suluhu katika
kulinda ndizi za kawaida zinazotumiwa kama chakula cha binaadamu zimeorodheshwa
miongoni mwa mimea inayoangamia.
Mti huo hupatikana nchini Madagascar pekee ambapo kuna miti
mitano iliosalia katika pori.
Wanasayansi wanasema kuwa mmea huo unahitaji kuhifadhiwa,
kwa kuwa huenda ukabeba siri za kulinda ndizi siku zijazo.
Changamoto ni kuanzisha aina mbali mbali ya ndizi ambazo ni
tamu kwa matumizi ya mwanadamu na ambazo zinaweza kustahimili mashambulio
yoyote kutoka kwa magonjwa ya Panama.
Ndizi ya Madagascar imekuwa pekee katika kisiwa na huenda
ina vitu muhimu.
Richard Allen, muhifadhi mwandamizi katika bustani ya Royal
Botanic, Kew, alisema kuwa aina yake huenda inaweza kustahimili ukame na
magonjwa.
"Haina ugonjwa wa Panama hivyobasi huenda ina vitu
muhimu vinavyoilinda dhidi ya magonjwa hayo," alisema.
"Hatujui hadi pale tutakapoifanyia utafiti ndizi hiyo,
lakini hatuwezi kufanya utafiti huo hadi itakapookolewa."
Wanasayansi wa Kew waliutafuta mti huo wa ndizi nchini
Madagascar na kugundua kwamba ulikuwa unaangamia duniani.
Hifadhi ya Maua
Wanatumai kwamba kuorodheshwa kwake miongoni mwa miti
inayoangamia katika shirika la umoja wa mataifa la IUCN (International Union
for Conservation of Nature utaangazia tatizo lake.
Dkt. Helene Ralimanana wa kituo cha uhifadhi nchini
Madagascar anasema kuwa mmea huo ni miongoni mwa urathi mkubwa wa kisiwa hicho.
"Ni muhimu kuhifadhi ndizi hizo za porini kwa sababu
zina mbegu kubwa ambazo zinaweza kutoa fursa ya kutafuta jeni ya kuimarisha
ndizi inayopandwa," alisema.
Iwapo ndizi hiyo inaweza kulindwa kutakuwa na fursa za
kukusanya mbegu zake na kuangalia jeni za mti huo.
Ndizi hiyo ya Madagascar inazalisha mbegu ndani ya tunda
hilo, hatua inayomaanisha kwamba haipendezi kula.
Lakini kuchanganya ndizi hizo mbili kunaweza kuzalisha aina
mpya ya ndizi ambayo inaweza kutumika na binadamu na vilevile kustahimili
magonjwa.
Ndizi hiyo hukuwa kandokando ya pori ambapo ni rahisi
kuharibiwa na hali mnbaya ya anga, ukataji wa miti, moto, mbali na kukata pori
kwa lengo la upanzi.
Kwa nini ndizi
zinaathiriwa rahisi na magonjwa?
Ndizi zinatoka katika eneo moja ikimaanisha kwamba zote ziko
sawa. Hivyobasi iwapo ugonjwa umepatikana katika mmea mmoja unaweza kuenea kwa
kasi katika mimea yote.
Tatizo ni lipi? Naweza
kununua ndizi katika duka
Kwa sasa hilo linawezekana lakini sio katika siku za usoni.
Ugonjwa unaoathiri ndizi ya Cavendish umedhibitiwa barani
Asia, na iwapo ungeenea nchini Marekani, ungeangamiza mmea wote wa ndizi.
Kila ndizi inayotumika kwa matumizi ya binaadamu inatoka
katika mmea huo.
Je, tunaijua ndizi ya
Madagascar?
Inajulikana kwa jina la kisayansi, Ensete perrieri, na imeorodheshwa kama mmea ulio katika hatari ya
kuangamia.
Inapatikana katika pori la misitu ya kitropiki katika eneo
la magharibi la taifa hilo ambapo inakabiliwa na hatari ya kukatwa kwa miti: Ni
miti mitano pekee inayodaiwa kusalia katika pori hilo.
Comments
Post a Comment