- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
EXUMA, BAHAMAS
KISIWA cha Exuma nchini Bahamas kina umaarufu wa michanga
meupe iliopo ufuoni mwa bahari , maji masafi na maneo mengi ya kuvutia.
Hivyobasi mwanamitindo Katarina Zarutskie alipozuru ufuo huo
pamoja na mpenzi wake, mwezi uliopita alikuwa na ari ya kutumia maeneo mazuri
ya fukwe hiyo ya bahari.
Baada ya chakula cha mchana na familia katika eneo
linalojulikana kama Staniel Cay, Katarina aliwaona watu waliokuwa wakiogelea
karibu na papa mchanga katika eneo moja.
Licha ya familia ya mpenzi wake kuwa na wasiwasi, alikuwa
yuko tayari kuingia katika maji hayo ili kupiga picha nao.
Msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 anatarajiwa kuanza
mafunzi ya shahada mbili za uuguzi na biashara mjini Miami na sio mgeni wa
maswala ya bahari baada ya kukuwa akifanya michezo ya baharini nyumbani kwao
huko mjini California.
''Kutokana na ufahamu wangu wa kuteleza majini na kuogelea
chini ya maji najua kwamba papa wachanga huwa salama'', aliambia BBC .
Nimeona watu wengi wakipiga picha nao katika mtandao wa
Instagram
Samaki huyo amekuwa kivutio cha watalii, akizurura katika
gati mbali mbali na kuonekana katika maelfu ya picha zilizosambazwa katika
mitandao.
Anasema kwamba baada ya dakika chache za kuchukua mkao, raia
mmoja wa eneo hilo alimshawishi kuolea majini huku mwili wake ukiangalia juu.
''Wakati huo watu walikuwa wameanza kupiga picha, nilipokuwa
nikilala kuangalia juu nilihisi kitu kimenivuta chini," alisema.
Babake mpenzi wake alikuwa akimpiga picha Katarina wakati
huo, na kwa bahati nzuri akapata kisa chote katika kamera yake.
Papa huyo alimzuilia chini ya maji kwa sekunde chache kabla
ya kuamua kuondoa kiganja chake cha mkono katika mdomo wake.
Picha hizo zinamuonyesha akifunika jereha hilo na kuinua
mkono wake katika juhudi za kuzuia damu kuenea katika maji .
"Wakati huo mwili wako una wasiwasi mwingi na hatua ya
pekee ni kujiondoa katika hali hiyo, lakini nilitulia," anasema.
"Nadhani iwapo mtu angepiga kelele na kuinua mikono
akitafuta usaidizi hali ingebadilika "
Katarina alilazimika kushonwa na kupewa dawa , na bado ana
vipande vya meno vya papa huyo vilivyosalia katika kidonda hicho.
Jeraha hilo la meno litawacha kovu baya , lakini
mwanamitindo huyo alisema kwamba anahisi amebarikiwa kwamba tukio hilo halikuwa
baya sana.
Tangu habari yake kuchapishwa katika vyombo vya habari vya
Marekani, Katarina amepokea maelfu ya mashabiki katika mtandao ikiwemo shutuma
chungu nzima
'Mwanamitindo mjinga wa instagram'.
Amekasirishwa na vile alivyodaiwa anapenda sana mitandao ya
kijamii bila tahadhari yoyote.
Mwanamitindo huyo hakupanga kupakia picha hizo katika
akaunti zake za mitandao ya kijamii hadi alipofuatwa na waandishi kuhusu uzoefu
wake wiki hii.
Katarina pia amepinga madai kwamba alipuuzilia mbali ushauri
wa wenyeji na kuingia majini wakati wa saa za kulishwa kwa wanyama hao.
''Walichukua habari walizotaka na kuchapisha kwa njia ambayo
zilinifanya kuwa mwanamitindo mjinga katika Instagram," alisema.
Nimepokea maoni ya ujeuri na ya chuki kutoka kwa wayu ambao
walikuwa wakisema vitu vya kushangaza.
Comments
Post a Comment