- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NEW YORK, MAREKANI
Mwanamke aliyekwea sanamu kubwa Marekani la Statue of
Liberty na kuketi yuko kuzuizini kwa mujibu wa polisi.
Watalii waliondolewa kutoka kisiwa cha Liberty kwenye
bandari ya New York Jumatano wakati wa sarakasi hiyo iliyodumu masaa matatu.
Ametajwa na vyombo vya habari vya Marekani Therese Okoumou,
mhamiaji wa miaka 44 kutoka DR Congo.
Bi Okoumou anaripotiwa kupinga sera za Trump zisizovumilia
uhamiaji.
Mapema watu kadha walukamatwa kwa kundamana kwenye sanamu
hiyo.
Wanachama wa kundi la wanaharakati Rise and Resist mapema
waliweka bango kwenye sanamu hiyo.
Polisi wa bustani na idara bustani mjini New York waliitwa
eneo hilo kufuatia ripoti kuwa mtu alikuwa akiikwea sanamu hiyo.
Baadaye Sarah akasema kuwa watalii walikuwa wakiondolewa.
Iliwachukua polisi saa tatu kumteremsha Bi Okoumou kwa
kutumia ngazi. Walisema wakuu wa mashtaka wataamua baadaye ikiwa atafunguliwa
mashtaka.
Brian Glacken wa idara ya polisi ya mjini New York alisema
haikuwa oparesheni rahisi.
Maandamano yamekuwa yakifanyika kote Marekani baada ya
taarifa kuibuka kuwa maajenti walikuwa wamewatenganisha maelfu ya watoto wadogo
kutoka kwa wazazi ambao wameingia Marekani kinyume na sheria.
Mwezi Februari waandamanaji waliweka bango kubwa lenye
maandishi "Karibu wahamiajia" kwenye sanamu hiyo.
Kutundika vifaa kwenye sanamu ya taifa, ambayo ni ishara ya
Marekani kukuwakubali wahamiaji, ni marufuku nchini Marekani, kwa mujibu wa
polisi wa bustani za taifa.
Comments
Post a Comment