- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
JOHANNESBURG, AFRIKA KUSINI
Takriban majangili wawili wa vifaru wame raruliwa na kuliwa
na simba katika mbuga ya wanyama huko Afrika ya kusini, maafisa wamesema.
Askari wa doria waligundua mabaki ya watu wawili, na wengine
wanahisi ni mabaki ya watu wa tatu, katika mbuga ya wanyama ya Sibuya karibu na
Kusini-Mashariki mji mwa mji wa Kenton.
Bunduki yenye nguvu kubwa na shoka pia vilikutwa hapo.
Katika miaka ya hivi karibuni, Ujangili umeongezeka sana
Afrika ya Kusini, ili kutokana na kuongezeka kwa hitaji la pembe za vifaru huko
bara la Asia.
Kwa upande wa China, Vietnum na sehemu nyingine nyingi pembe
za vifaru zinaaminika kuwa na sifa ya kuongeza hisia za mapenzi.
Mmiliki wa Hifadhi wa Sibuya, Nick Fox katika taarifa yake
kwenye ukurasa wa Facebook wa mbuga hiyo amesema watu hao wanao sadikiwa kuwa
ni majangiri waliingia katika mbuga hiyo jumapili usiku au mapema siku ya
Jumatatu asubuhi.
"Walikosea na kuingia kwenye eneo la kujidai la simba,
ni eneo kubwa hivyo hawakuwa na muda mwingi, " Bwana Fox aliliambia
Shirika la habari la AFP.
"Hatuna hakika ni watu wangapi walikuwa - kwani kuna
mabaki kidogo sana ya miili yao. "
Mabaki hayo ya likutwa majira ya saa 16:30 siku ya Jumanne.
Timu ya kupambana na ujangili iliwasili katika eneo la
tukio, sehemu ambapo bunduki ya uwindaji yenye kifaa cha kuzuia sauti, shoka
refu na waya - vifaa ambavyo hutumiwa na majangili vilipatikana.
Ili kupatikana kwa mabaki ya watu hao, ilibidi simba kadhaa
kuchomwa dawa za usingizi, bwana Fox aliongeza.
Hata hivyo, Polisi wanaendelea na kupiga doria katika eneo
hilo ili kuangalia kama kuna majangili walio nusurika ku uawa na simba hao.
Kwa mwaka huu pekee, Vifaru tisa waliuawa na majangili
mashariki mwa jimbo la Rasi, sehemu ambayo hifadhi hiyo ipo.
Hata hivyo, zaidi ya faru 7,000 wameuawa nchini Afrika
Kusini katika muongo uliopita pekee.
BBC/SWAHILI
Comments
Post a Comment