- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
KAMPALA, UGANDA
SERIKALI ya Uganda imetangaza kwamba tozo la kodi ya
mitandao ya kijamii huduma ya kutuma pesa kwa simu itaangaliwa upya.
Kodi hiyo ya shilingi 200 za Uganda ambayo ni sawa na $0.05
inayotozwa ili mtu aweze kutumia mitandao kama Twitter na Facebook imechangia
kuzuka maandamano nchini.
Lakini hakuna hakikisho kuwa kodi hiyo itaondolewa na huenda
ikachukua wiki kadhaa kabla ya kuidhinishwa mageuzi yoyote yale.
Baadhi ya wabunge wanashinikiza kodi hiyo isitishwe kwa
muda.
Bunge litajadili hatua inayofuata leo.
Mapema jana Jumatano Polisi nchini imefyatua gesi ya kutoa
machozi na risasi hewani kutawanya kundi la waandamanji wanaopinga kodi
iliyoidhinishwa ya kutumia mitandao ya kijamii.
Mwandishi wa BBC anasema polisi wamejaribu kumkamata mbunge
ambaye pia ni muimbaji mashuhuri Robert Kyagulany, anayefahamika kwa umaarufu
Bobi Wine, aliyeongoza maandamano hayo, lakini amefanikiwa kutoroka.
Mpiga picha mmoja katika maandamano hayo amekuwa akituma picha
katika mtandao wa kijamii Twitter kuhusu yanayoendelea:
Kodi hiyo iliyoidhinishwa mwanzoni mwa mweiz huu inahitaji
watumiaji mitandao ya kijamii nchini kulipa shilingi 200 za Uganda [$0.05,
£0.04] ili waweze kutumia mitandao kama Facebook, Twitter na WhatsApp.
Ni kwanini serikali inatoza kodi hii ?
Bunge liliidhinisha kodi hiyo mnamo Mei baada ya rais Yoweri
Museveni kushinikiza mageuzi hayo.
Rais Museveni a anaoutaja kuwa maoni, upendeleo, matusi na
hata chati kwa marafiki.
Katika barua aliyomuandikia waziri wa fedha mnamo Machi,
rais Museveni amesema kodi kwa mitandao ya kijamii inaweza kuongeza kipato cha
serikali, na kupunguza mikopo inayochukua serikali na pesa za ufadhili.
Ameongeza kwamba haungi mkono kodi iitozwe kwa matumizi
jumla ya mtandao kwasababu hili litaathiri matumizi yake kwa misingi ya 'elimu,
na utafiti '.
Waziri wa habari na mawasiliano Uganda Frank Tumwebaze pia
ametetea kuidhinishwa kwa kodi hiyo, akisema kwamba fedha zitakazopatikana
zitatumiwa 'kuwekeza katika rasilmali zaidi za kimitandao'.
Lakini baadhi wanalalamika kuwa hii ni njia ya kubana au
kuzuia kauli zinazoikosoa serikali.
Inakadiriwa kwamba zaidi ya asilimia 70 ya raia nchini
Uganda wana simu za mkononi.
Ni 41% ya raia nchini wanatumia mtandao Uganda kufikia
mitandao ya kijamii kama Facebook na Twitter iliyo maarufu zaidi nchini humo.
Haya ni kwa mujibu wa utafiti wa kitaifa wa mamlaka ya
habari na taknolojia Uganda (NITA-U).
Mataifa mengine Afrika mashariki katika siku za hivi
karibuni yamepitisha sheria za kudhibiti matumizi ya mitandao ambazo wakosoaji
wanasema zinaathiri uhuru wa kujieleza.
Comments
Post a Comment