- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
BERLIN, UJERUMANI
MAHAKAMA ya juu nchini Ujerumani imeamuru kuwa wazazi wa
binti aliyefariki wapate haki za kuingia kwenye akaunti ya Facebook ya binti
yao, kwa mujibu wa sheria za mirathi nchini humo.
Mahakama hiyo imesema data za mtandaoni zipewe hadhi sawa
kama vile ilivyo kwa barua binafsi au kumbukumbu nyingine binafsi na
kurithishwa kwa wanafamilia.
Shauri hili lilihusisha wazazi wa binti wa miaka 15
aliyepoteza maisha kutokana na kuigonga treni mwaka 2012.
Walitaka kibali cha kuingia kwenye anuani yake ya Facebook
ili waweze kufanya uchunguzi kubaini kama binti yao alidhamiria kujitoa uhai.
Facebook ilikataa kutoa kibali baada ya kifo cha binti huyo,
ikijitetea kuwa hiyo ni anuani ya mtu binafsi.
Sera mpya za Facebook, Kampuni inaruhusu wanafamilia, walezi
kuingia na kuitumia kwa kuruhusu kubadili ukurasa kwa ajili tu ya maombolezo
mtandaoni au kuifuta kabisa (after-death controls).
Mahakama ndogo iliwaunga mkono wazazi mwaka 2015, ikieleza
kuwa data za muhusika katika Facebook ziko kwenye sheria ya mirathi.
Lakini mwaka 2017, Facebook ilishinda rufaa kwa misingi kuwa
mkataba kati ya binti na Kampuni ulikwisha baada ya kifo, hivyo mkataba huo
hauwezi kuhamishiwa kwa wazazi.
Shauri lilifikishwa kwenye mahakama kuu na sasa wazazi
wameripotiwa kuhodhi anuani hiyo.
Jaji wa mahakama hiyo, Ulrich Hermann, alisema ni kawaida
kurithisha vitu kama barua na maandiko mengine ya marehemu kwa familia na haoni
sababu ya anuani ya digitali itazamwe tofauti.
Zaidi ya hayo mahakama imesema wazazi wana haki ya kufahamu
mtoto wao alikuwa anawasiliana na nani.
Ni kwa jinsi gani
unapenda kukumbukwa utakapofariki?
Miezi micheche kabla ya kupoteza maisha, Bibi yangu alifanya
uamuzi.
Bobby, kama alivyokuwa akiitwa na marafiki zake (kwao ni
kizazi cha majina ya a.k.a) alikuwa mke wa mkulima ambaye si tu alinusurika
katika vita ya pili ya dunia lakini pia alikuwa mahiri wa kutunza vitu, ilikuwa
ni taratibu za kuishi alizojiwekea baada ya Uingereza kurejea katika uimara
wake baada ya vita.
Hivyo aliendelea kutunza bahasha na makaratasi yanayotokana
na maboksi ya vyakula kwa ajili ya kuandikia na kunakili orodha mbalimbali.
Alitunza pia picha za watu wa familia yake, aliendelea
kutunza barua za mapenzi alizokuwa akitumiwa na babu yangu alipokuwa safarini. Nyumba
yake ilikuwa na kumbukumbu nyingi sana.
Katika miezi michache kabla ya kifo chake, mwelekeo
ukabadilika kumbukumbu zote zikaanza kutolewa. Kila mara nilipomtembelea
hulijaza gari langu na vitu mbali mbali, katoni za juisi ya machungwa, vitabu,
bilauri.
Kumbukumbu zote alianza kuzitoa nyumbani. Alituma picha
zilizofifia kwa watoto wake, wajukuu na marafiki, zikiwemo barua zilizoandikwa
zikiwa na aya ambazo wazi kabisa zilieleza aliyoyapitia maishani na mambo
mengineyo.
Aprili 9, 2018 usiku kabla ya kifo chake alituma barua kwa
marafiki wa utotoni wa marehemu mumewe.
Kwenye bahasha aliambatanisha picha za babu yangu na rafiki
yake wakicheza walipokuwa watoto, aliandika ''Lazima uwe nazo,'' aliandika
ilikuwa kama amri lakini pia ombi, labda akimaanisha vitu hivi si vya
kuvipoteza au kuvisahau. Saa chache baadae alifariki akiwa kwenye kiti chake
alichokipenda sana.
Siku hizi tunatunza kumbukumbu zetu kwenye intaneti. Kuna
Facebook ambayo hurekodi matukio yetu muhimu ya maisha, Instagram ambapo
tunatunza tunayoyapenda, Gmail ambayo hutunza mazungumzo yetu na YouTube ambayo
hutangaza namna tunavyoendelea, tunavyozungumza na tunavyoimba. Tunakusanya
kumbukumbu hizi ziweze kuishi muda mrefu.
Je inatosha? Tunatunza kile tunachoamini kuwa ni muhimu,
lakini je kama tunakosa vitu vilivyo muhimu? Inakuwaje kama tunakosa kitu
muhimu kwenye maneno yetu au kwenye picha zetu?
Ni kwa namna gani inaweza kuwa vyema kutunza kila kitu, si
tu mawazo yetu kwa maandishi na picha zinazoonyesha maisha yetu, lakini mawazo
yetu yote akilini: Kila kitu tunachokijua na vyote tunavyovikumbuka, mambo ya
mapenzi na kuvunjika moyo, nyakati za ushindi na masikitiko, uongo tunaoueleza
na ukweli tunaojifunza, ungeweza kuhifadhi kila kitu kichwani kama kwenye mfumo
wa kompyuta?
Kuna wahandisi wanafanyia kazi teknolojia ambayo itaweza
kutengeneza kopi za akili zetu na kumbukumbu zitakazoishi hata baada ya kifo.
Karatasi ya Kaboni
Ninatunza barua za Bibi kwenye kablasha lililo kwenye meza
yangu. Pia nina picha zake kwenye ukuta jikoni kwangu, na vile vitabu vya
zamani ambavyo vimekuwa vikuukuu vikiwa bado havijasomwa. Hizi ni njia ambazo
ninamkumbuka na kumbukumbu zake nimezitunza kwenye makaratasi.
Lakini ningeweza kufanya zaidi kutunza kumbukumbu hii?
Bibi wa Aaron pia alifariki hivi karibuni. ''Kilichonishtua
ni kuwa ni kwa namna ambavyo hakuna kumbukumbu za kutosha zilizobaki,'' Mjukuu
wake mwenye miaka 30 ananiambia ''ameacha vitu vyake vichache. Nina shati lake
la zamani ambalo huwa ninalivaa ninapokuwa nyumbani."
Kifo chake kilimhamasisha kujiunga na taasisi ya Eterni.me huduma ya mtandao ambayo
huhakikisha kumbukumbu za mtu aliyefariki zinatunzwa mtandaoni.
Inafanya kazi hivi:
Wakati ukiwa hai unaipa kibali taasisi hiyo kuweza kuingia
kwenye mtandao wako wa Facebook, Twitter na anuani za barua pepe, weka picha na
kuonyesha maeneo mbalimbali ulipokuwa na vitu ulivyoviona, data hurekodiwa,
kuchujwa na kuchambuliwa kabla ya kupelekwa kwenye teknolojia ya Avatar ambayo
itakuwa ikikusoma kadiri unavyoendelea kuishi.
''Ni katika kuepuka hali ya kutokumbukwa siku za usoni,"
anasema Marius Ursache mmoja kati ya wabunifu wa Eterni.
''Wajukuu wa wajukuu zako watazitumia kumbukumbu zako, kwa
mfano picha za familia, mawazo yako, matukio ya kukumbukwa ya familia na mawazo
yako kuhusu mada mbalimbali na hata nyimbo ulizowahi kuimba lakini
hazikuchapishwa."
CHANZO: BBC
Comments
Post a Comment