- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
UGONJWA usiojulikana sana wa zinaa unaibuka kuwa usiosikia
dawa ikiwa watu hawatakuwa waangalifu, wataalamu wameonya.
Ugonjwa huo unaojulikana kama Mycoplasma genitalium (MG)
hauna dalili lakini unaweza kuwa na madhara ikiwemo kusababisha utasa kwa
wanawake.
MG unaweza kukoswa kutambuliwa na kama hautatibiwa vizuri
unaweza kuwa sugu kwa madawa.
Shirika la Uingereza linalohusika na afya ya ngono na HIV
limeznzisha shuguhli ya kutoa ushauri.
Nakala yake inalaeza jinsi ya kutambua na kutibu ugonjwa wa
MG.
MG ni ugonjwa gani? Mycoplasma genitalium ni bakteria ambayo
inaweza inaweza kuambukiza wanaume na kuathiri uume kusababisha vigumu
kupitisha mkojo.
Kwa wanawake inaweza kuathiri sehemu za uzazi na kusababisha
uchungu na hata kuvuja damu.
Ugonjwa huu unaweza kuambukizwa kwa njia ngono isiyo na
kinga kutoka kwa mtu ambaye tayari ana ugonjwa huo, Mpira wa kondomu unaweza
kuzuia maambukizi.
Mara ya kwanza ugonjwa huu ulitambuliwa nchini Uingereza
mwaka 1980 na unaaminika kuwaathiri asilimia moja au mbili ya watu wote.
MG mara nyingi hauna dalili na hautaji wakati wote matibabu
lakini unaweza kukosa kutambuliwa au kuchukuliwa kuwa ugonjwa tofauti.
"Matumizi wa kondomu"
Kuangamziwa ugonjwa wa MG kwa kutumia aina moja ya dawa
inayofahamika kama macrolides, kumeshuka kote dunaini. Usugu wa ugonjwa huu
unakadiriwa kufikia asilimia 40 nchini Uingereza.
Hata hivyo dawa moja inayojulikana kama azithromycin bado
inautibu mara nyingi.
Dkt. Peter Greenhouse, mshauri wa masuala ya ngono huko
Bristol anawashauri watu kuchukua tahadhari.
"Ni wakatai ambapo watu wanafahamu kuhusu Mycoplasma
genitalium," alisema.
"Kuna sababu nzuri ya kubeba kondomu wakati wa likizo
za msimu wa joto na kuzitumia."
Comments
Post a Comment