- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Baadhi ya watumiaji wa mtandao wa Twitter wamewasilisha
maombi yao ya kutaka kuolewa na mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote,
baada ya gazeti la Uingereza Financial Times kuripoti kwamba anatafuta mke.
''Umri wangu haupungui. Miaka sitini sio mzaha.... Lakini
haiingii akilini kwenda kutafuta mtu iwapo huna muda huo," Dangote
aliambia gazeti hilo.
''Hivi sasa sina wakati kwa sababu tuna kiwanda cha
kusafishia mafuta, tuna kemikali za mafuta, tuna mbolea, tuna bomba la
kusafirishia gesi," bwana Dangote alisema, akiongezea: Nahitaji kutulia
kidogo.
Lakini baadhi ya watu walikasirishwa na lengo la mahojiano
na tajiri huyo kuhusu maisha yake ya kibinafsi.
Dangote amewahi kuwaoa wanawake wengi ingawa habari kuwahusu
wanawake wanaohusishwa naye huwa vigumu kuzithibitisha.
Hata hivyo, inafahamika kwamba aliwapa talaka wake wawili.
Ana watoto watatu walioorodheshwa rasmi, maarufu akiwa ni
Halima Dangote aliyefunga ndoa mapema mwaka huu katika sherehe ya harusi
iliyohudhuriwa na watu mashuhuri duniani akiwemo mwanzilishi wa Microsoft
bwanyenye Bill Gates na Rais wa zamani wa Tanzania Jakaya Kikwete. Watoto hao
wengine ni Fatima na na Mariya.
Yeye ni Mwislamu na dini yake inamruhusu kuwaoa wake wengi.
Hata hivyo, licha ya kuwa na wake wengi taarifa zinasema hajawahi kuwa na zaidi
ya mke mmoja kwa wakati mmoja. Kwa sasa, watu wamekuwa wakimchukulia kuwa asiye
na jiko.
Aliko Dangote ni nani?
Aliko Dangote ndiye mtu tajiri zaidi mweusi duniani na mtu
tajiri zaidi Afrika.
Alianzisha kampuni ya Dangote Cement na bado ndiye
mwenyekiti wa kampuni hiyo. Dangote Cement inaongoza kwa kutengeneza saruji
Afrika.
Dangote pia anamiliki kampuni za sukari, chumvi na za kusaga
unga.
Kampuni yake ya Dangote Group inajenga kiwanda cha kusafisha
mafuta karibu na Lagos, Nigeria ambacho kitakapomaliza kujengwa mwaka 2019
kinatarajiwa kuwa kikubwa zaidi cha aina yake duniani. Kiwanda hicho
kitagharimu $9bn.
Dangote amehifadhi taji la kuwa mtu mweusi tajiri zaidi
duniani akiwa na utajiri wa takriban $14.1 bilioni.
Comments
Post a Comment