- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
QUEENSLAND, AUSTRALIA
WENYE magari katika eneo moja nchini Australia wamelazimika
kuyaacha magari yao baada ya lami kuanza kuyeyuka barabarani.
Tairi za magari ziliharibiwa vibaya na lami na sasa madereva
takriban 50 wanadai fidia.
Kisa hicho kilitokea katika jimbo la Queensland siku ya
Jumanne.
"Sijawahi kuliona jambo kama hili maishani na taarifa
zilipoaza kutolewa jana, lilikuwa jambo la kushangaza sana," meya wa eneo
hilo Joe Paronella ameambia ABC.
Maafisa wanasema kisa hicho kilisababishwa na jua kali,
pamoja na hali kwamba ukarabati ulikuwa umefanyika wiki iliyopita.
Mkazi mmoja wa eneo hilo Deborah Stacey anasema tairi za
magari zilijawa na lami.
Jua kali lilikuwa limewaka baada ya siku kadha za mvua.
"Tulishuhudia wiki ya vioo vya magari kuharibiwa na
mvua ... kisha jua lilipochomoza, tunashuhudia haya sasa," ameambia jarida
la Courier Mail.
Barabara hiyo inapatikana katika eneo la Atherton Tablelands
kusini mwa mji wa Cairns na ilifungwa kwa muda.
Wizara ya uchukuzi ya jimbo la Queeensland imeahidi kwamba
watu ambao magari yao yaliharibika watalipwa fidia.
Barabara huyeyuka
wakati gani (Uingereza)?
•Lami kwenye barabara nyingi huweza kuyeyuka kiwango cha
joto kikifikia 50C
•Takriban 5% ya barabara 80C
•Barabara za lami hushika joto sana na hivyo kiwango chake
cha joto kinaweza kufikia 50C jua kali likiwaka.
Comments
Post a Comment