- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NAIROBI, KENYA
Glorious Amani, Msichana wa eneo la Githurai nchini Kenya
aliyelishangaza taifa kwa namna alivyoimba wimbo wa nyota wa muziki kutoka
Marekani Alicia Keys amesajiliwa na kampuni ya muziki.
Amani amesajiliwa na kampuni ya Pine Creek Records iliopo
jijini Nairobi ambayo imeamua kukuza kipaji chake.
Kampuni hiyo ya muziki ilitangaza habari hiyo njema katika
mtandao wake wa facebook.
Akizungumza na BBC kwa njia ya simu, Afisa mkuu wa kampuni
hiyo Peter Nduati amesema kuwa msichana huyo atakayetia saini kandarasi ya
miaka miwili atazinduliwa rasmi siku ya Ijumaa
Nduati amesema kuwa mamake msichana huyo atahudhuria hafla
hiyo.
''Kipaji chake kimewasili nyumbani ambapo kitakuzwa kwa
kiwango cha juu... Jumuika nasi katika kumkaribisha Amani G katika lebo yetu ya
muziki'', ulisema ujumbe huo katika mtandao wa Facebook.
Baadaye kanda fupi ya video inamuonyesha msichana huyo akiimba
wimbo mmoja wa kiswahili usiojulikana.
Amani aligonga vichwa vya habari mwezi uliopita baada ya
video yake inayomuonyesha akiimba wimbo wa nyota wa muziki nchini Marekani
Alicia Keys kusambazwa sana mitandaoni.
Alicia Keys baadaye alituma ujumbe wa Twitter kuhusu kanda
hiyo ya video akisema ni msichana mrembo.
Mwanamuziki wa Kenya Vivian amerekodi wimbo mmoja naye.
Amani ambaye yuko katika darasa la nane ni mwana wa Wuod
Fibi, mwimbaji wa Kenya na mtayarishaji wa muziki. Pia amejipatia jina Amani G.
Comments
Post a Comment