- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA
MWANDISHI WETU, ZANZIBAR
CHAMA cha
The Alliance African Farmers for Tanzania (AAFP ) kimesifu uamuzi wa Rais Dkt.
John Magufuli kukutana na viongozi wastaafu wa serikali zote mbili na kuwataka
watoe maoni, ushauri na mitazamo yao ni zaidi ya moyo wa chuma huku akitaka nchi ifike mbali kimaendeleo.
Kimesema
hatua hiyo licha ya kufungua milango na serikali ikitaka kuchota maoni, ushauri na kuondosha baadhi ya
kasoro pia imelenga kujenga haiba ya mapatano hivyo ni vyema pia akakutana na
viongozi wa vyama vya siasa.
Ushauri
huo umetolewa juzi na Mwenyekiti wa Taifa wa AAFP, Said Soud Said, huko Mombasa
kwenye Ofisi za chama hicho akisema mkutano uliowakutanisha viongozi wastaafu
wa serikali kwa sehemu kubwa utaondosha au kupunguza joto la mshawasha,
sintofahamu na upekepeke.
Soud
alisema, Rais Magufuli amewapa jukwaa la wazi wastaafu hao ili wafunguke kwa
kutema nyongo, kushauri, kutoa maoni na mitazamo yao hivyo kama yupo aliyeogopa
na baadaye atake kusema kwenye vibuyu, atakuwa hajafanya uungwana.
Alisema
kikao kile kilikuwa na umuhimu wa pekee kwani kila kiongozi alipaswa kueleza
kwa kadri anavyofikiri, kupendekeza, kushauri lakini pia kukosoa iwapo zipo
hitilafu na dosari za kiutawala zinazaoonekana kuchomoza au kwenda ndivyo
sivyo.
"AAFP
inasifu uamuzi wa Dkt. Magufuli kukutana na viongozi wastaafu wa serikali zote
mbili. Ameunda jukwaa la wazi akiwataka wafunguke. Ameonyesha ujasiri na uwazi
wa serikali yake kupokea maoni. Ipo haja sasa akakutana na viongozi wa vyama vya
siasa," alisema Soud.
Aidha,
Mwenyekiti huyo alisema Rais Magufuli amesifu misingi iliyowekwa na watangulizi
wake katika ujenzi wa nchi, hivyo akataka apate ushauri mpya iwapo ndani ya
miaka yake miwili na ushee akiwa madarakani kama kuna dosari na hitilafu ili
serikali yake ijiweke sawa.
"Hakuna
mtawala Kusini mwa Afrika aliyethubutu kuitisha kikao kama kile. Amekuwa na
moyo wa chuma akitaka kukusanya mawazo ya pamoja katika ujenzi wa nchi. Kama
yupo kiongozi mstaafu aliyeshindwa kushauri lolote au kukosoa, huyo hakutimiza
wajibu wake," alieleza.
Alisema
ingawaje katika mkutano na viongozi wa vyama vya siasa atakabiliana na
wapinzani wake kisera, vyama pinzani vina wajibu wa kujenga indhar ya ushauri
wenye nguvu ya hoja badala ya propaganda kwani Rais aliye madarakani muda wake
wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi haujamalizika.
"Kiwe
ni kikao cha ushauri na ukusanyaji maoni kisiwe cha malumbano wala mipasho ya
kisiasa. Yatupasa wote tujiandae kimkakati kushauri na kama zipo dosari zinazohitaji
makemeo ya kisiasa, vyama visubiri mwaka 2020 au watumie kampeni za chaguzi
ndogo za katika majimbo ya Jang'ombe na Buhingwe," alieleza.
Pia
Mwenyekiti huyo wa AAFP alisema kitendo cha kuwaita watangulizi wake akiwataka
watoe mitazamo na fikara zao ni katika namna ya mbinu za kiongozi kutaka aidha
kujipima, kujisahihisha na kujipanga zaidi ili Taifa liwe na mshikamano badala
ya kuishi kwa mivutano isio na tija.
"Ikiwa
vitendo vya ufisadi, rushwa na maonevu vinazidi kupungua, wafanyakazi kwenye
taasisi za umma wanatoa huduma kwa nidhamu, Serikali inakusanya kodi huku
huduma za jamii zikiboreshwa, lazima anayeshauri awe na mawazo mbadala na si
porojo," alisisitiza.
Hata hivyo,
Soud alisema viongozi wastaafu walioitwa kushiriki kikao kile ni wakongwe na
wabobezi katika medani za siasa, utawala na uongozi, hivyo ushauri wote waliotoa mbele ya Rais
bila shaka utachukuliwa na serikali kwa umuhimu na kupewa kipaumbele.
Comments
Post a Comment