- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA MWANDISHI WETU
SHIRIKISHO la Soka Africa (CAF) limetaja waamuzi kutoka Somalia
ambao ndio watachezesha mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya makundi kati ya
Gor Mahia ya Kenya na Yanga utakaochezwa Uwanja wa Moi Kasarani, Nairobi Julai
18, 2018.
Kwenye mchezo huo, Mwamuzi wa katikati atakuwa Hassan
Mohamed Hagi akisaidiwa na Hamza Hagi Abdi, Suleiman Bashir Sh.Abdi na Mwamuzi
wa akiba atakuwa Nur Muhidin Mohamed.
Taarifa ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imesema kuwab, Mtathmini
waamuzi atakuwa Jan Olivier Mbera kutoka Gabon na Kamishna wa mchezo ni Simphiwe
Brian Xaba kutoka Afrika Kusini atakayeongozana na na mratibu wa mchezo huo,
Nomsa Jacobeth Mahlangu.
Aidha, mchezo wa marudiano kwa timu hizo utakaochezwa Julai
29, 2018 kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam wenyewe utachezeshwa na waamuzi
kutoka Mauritius.
Mwamuzi wa katikati atakuwa Ahmed Imtehaz Heeralall
akisaidiwa na Cauvelet Louis Ralph Fabian na Akhtar Nawaz Rossaye, na Mwamuzi
wa akiba atakuwa Ganesh Chutooree.
Kamishna wa mchezo atakuwa Patrick Kangwa kutoka Zambia,
Mtathmini waamuzi ni Louzaye Rene Daniel kutoka Congo wakati Mratibu atakuwa Nasiru
Sarkintudu Jibril kutoka Nigeria.
Comments
Post a Comment