- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
NA JANE
MWAKYOMA, RUKWA
Wananchi
wa mwambao wa ziwa Tanganyika wameishukuru serikali kwa kutenga fedha bilioni 3
kwa ajili ya upanuzi wa Bandari ya Kasanga ili kukuza pato la taifa.
Wakizungumza
kwa nyakati tofauti baada ya Mkurugenzi wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA),
Deus Kakoko, kufanya ziara katika vijiji vinavyozunguka Ziwa Tanganyika wilayani
Kalambo, walisema uongozi wa awamu ya tano umekuwa ukisikiliza kilio cha
wananchi wa hali ya chini ususani wananchi wa mwambao mwa Ziwa Tanganyika
ambapo serikali imeona umuhimu wa kupanua Bandari ya Kasanga ambayo imekuwa ni muhimu sana kwa wakazi wa
mkoa wa Rukwa na imekuwa ikiingizia serikali mapato kutokana na biashara
zinazofanyika bandarini hapo.
Walizitaja
furusa zitakazowanufaisha wakazi hao wakati wa mladi kuanza na mara baada ya
mladi kumalizika ambapo walizitaja furusa hizo wakati wa ujenzi kuanza ambapo
wananchi hao walisema watapa ajira wakati wa ujenzi wa bandari hiyo,na biashara
itakua ikiwa ni pamoja na kukua kwa kipato cha
mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla ambapo biashara hiyo itaambatana na
uvuvi wa kisasa kutokana na upanuzi wa bandari hiyo.
Walisema
upanuzi huo utasaidia kuongezeka kwa meli za kisasa kubwa ambapo meli hizo
zitasaidia mwingiliano wa biashara na kupanuka kwa biashara zitakazokuwa
zikifanyika bandarini hapo ambapo ziwa Tanganyika linapakana na nchi kama Jamuhuri
ya Kidemokrasia ya Congo na nchi ya Zambia ambao ni wafanyabiashara wakubwa
wanaotumia Bandari ya Kasanga kutokana na ushirikiano ambao unafanywa na nchi
hizo wa kubadilishana biashara bandarini hapo.
Mkurugenzi
wa TPA, Deus Kakoko, alisema ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami
umemalizika ambapo alisema kilichobaki ni kutafuta mkandarasi ambaye atajenga
bandari hiyo ambapo bandari hiyo imekuwa finyu kutokana na kupanuka kwa
biashara ambapo serikali imeona umuhimu wa kujenga bandari ambapo bandari hiyo
itakuwa kubwa na yakisasa ili kuongeza kasi na mwingiliano wa biashara
bandarini hapo.
Alisema
wananchi wa mwambao mwa ziwa Tanganyika ni wakati wao kuchangamkia furusa
zitakazotokana na ujenzi wa Bandari ya Kasanga ambapo wakazi watapata ajira,na
biashara kupanuka ambapo hoteli za kisasa zitajenga na wakazi watapata ajila
kutokana na huduma zitakazobareshwa
katika eneo hilo na biashara nyingi zitakuwa na kukuza pato la taifa nchini.
Alisema
pamoja na upanuzi wa Bandari ya Kasanga pia kutakuwepo na biashara haramu
ambapo aliziagiza mamlaka husika kuwa makini na mizigo itakayokuwa inaingia
bandarini hapo ili kuepusha nchi yetu kuwa na biashara ambayo si harali na
inaweza kuleta madhara kwa jamii,
"Tunatarajia
meli kubwa zitakuwa zinaleta mizigo na kusafirisha mizigo, sasa kuna boti
tutafurahia upanuzi wa bandari lakini tuangalie na kuchunguza mizigo inayotoka
na kuingia, mtu anaweza kutumia boti kusafirisha biashara ambayo si harali na
mwisho wa siku biashara hiyo unaikuta mitaani, naagiza kila mtu afanye kazi
yake usiku na mchana," alisema Deus Kakoko.
Comments
Post a Comment