- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
MOSCOW, RUSSIA
KUNA mataifa 32 yanayoshiriki Kombe la Dunia, lakini mshindi
atakuwa mmoja. Je, unawezaje kubashiri nani atainua Kombe la Dunia mjini Moscow
15 Julai?
Kwa kuangalia mtindo, takwimu na yaliyotokea katika
mashindano ya awali, BBC Sport imeondoa mataifa 31 na kusalia na taifa moja
ambalo kwa mujibu wa vigezo hivyo ina nafasi kubwa zaidi ya kuwa mabingwa wa
dunia.
Hapa kuna mambo ambayo mshindi wa Kombe la Dunia wa mwaka
2018 anafaa kutimiza:
Awe wa kwanza kwenye
chungu
Tangu Kombe la Dunia lilipopanuliwa na kuwa na timu 32 mwaka
1998, mabingwa wote walikuwa ni taifa ambalo lilikuwa la kwanza kwenye chungu
wakati wa kufanyika kwa droo.
Timu ya mwisho kushinda bila kuwa kwenye chungu ilikuwa ni
mwaka 1986 Argentna waliposhinda wakiwa na Diego Maradona na bao lake la 'mkono
wa Mungu'. Kwa kutumia kigezo hicho, tumeondoa mataifa 24 ambayo yanashiriki
mashindano hayo mwaka huu, na kusalia na timu nane.
Usiwe mwenyeji
Urusi imefaidika kushiriki michuano hiyo kwa sababu ya kuwa
taifa mwenyeji.
Kumekuwa na utaratibu kwamba taifa mwenyeji lazima liwe
kwenye chungu. Hilo limekuwepo kwa miaka 44.
Lakini ukizingatia kwamba nafasi yao kwenye orodha ya
viwango vya soka duniani ya Fifa ni 66, hawangekuwa miongoni mwa nchi hizo nane
za kuwekwa kwenye chungu kama hawangekuwa wenyeji.
Kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia siku hizi pia si hakikisho
kwamba utafanya vyema kama ilivyokuwa zamani.
Katika makala 11 ya michuano hiyo, 1930 hadi 1978, mara tano
mwenyeji ndiye aliyeshinda.
Tangu wakati huo, katika michuano tisa iliyochezwa karibuni
mwenyeji alishinda mara moja pekee - Ufaransa 1998.
Ingawa ni kweli hakukuwa na matarajio yoyote kwamba
Marekani, Japan, Korea Kusini au Afrika Kusini wangeshinda Kombe la Dunia,
Italia mwaka 1990, Ujerumani mwaka 2006 na Brazil miaka minne iliyopita ni
mataifa ambayo yalitarajiwa kushinda wakiwa wenyeji. Lakini hawakufanikiwa.
Usifungwe mabao mengi
Katika enzi hii ya timu 32, mabingwa wote watano
hawajafungwa zaidi ya magoli manne katika mechi saba walizocheza.
Ukiangalia timu saba tulizosalia nazo, Poland ndio walio na
safu ya ulinzi hafifu zaidi ukiangalia mechi zao za kufuzu, walifungwa bao 1.4
kwa kila mechi.
Ujerumani na Ureno walifungwa 0.4 kila mechi, Ubelgiji na
Ufaransa 0.6, Brazil 0.61 na Argentina 0.88.
Uwe kutoka Ulaya
Washindi wa Kombe la Dunia kufikia sasa wote wametokea Ulaya
na Amerika Kusini. Hadi miaka ya karibuni, timu za Ulaya zilikuwa hazisafiri
mbali kwa mechi hizo. Lakini ufanisi wa Uhispania nchini Afrika Kusini na
Ujerumani nchini Brazil umeonesha kwamba wanafanikiwa hata wakisafiri mbali.
Michuano inayoandaliwa Ulaya, hata hivyo, mara nyingi
hushindwa na wenyeji. Kati ya michuano 10 iliyoandaliwa na nchi kutoka Ulaya,
ni moja pekee ambayo mshindi alikuwa wa kutoka nje.
Na inakulazimu kurudi nyuma hadi mwaka 1958 Brazil
waliposhinda michuano iliyoandaliwa Sweden.
Kuwa na kipa bora
zaidi
Unaweza ukafikiria kwamba wafungaji mabao ndio husaidia
mataifa kushinda Kombe la Dunia, lakini ni mara mbili pekee tangu 1982 ambapo
mshindi alikuwa na mfungaji mabao bora.
Mwaka 2002 Brazil iliposhinda ikiwa na Ronaldo na David
Villa na Uhispania mwaka 2010.
Washindi wa Kombe la Dunia zaidi husaidiwa na walinda lango
wao.
Washindi mara nne kati ya tano wa kipa bora wa michuano
walikuwa magolikipa wa timu ambayo iliibuka mshindi mwishowe.
Kati ya mataifa manne yaliyosalia, si vigumu kufikiria mmoja
kati ya Manuel Neuer (Ujerumani), Hugo Lloris (Ufaransa) au Thibaut Courtois
(Ubelgiji) akitawazwa kipa bora zaidi wakati huu.
Uwe na uzoefu
Mataifa yaliyoshinda Kombe la Dunia yamekuwa na wachezaji
ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa na uzoefu. Ni mtindo ulioanza michuano hii
ilipopanuliwa na kuwa na timu 32 mwaka 1998.
Wakati huo, mabingwa Ufaransa walikuwa na kikosi cha wachezaji
ambao kwa wastani walikuwa wamechezea taifa mechi 22.77 kwa wastani.
Miaka minne iliyopita, mabingwa Ujerumani walikuwa na uzoefu
wa mechi 42.21.
Hapo katikati kulikuwa na kuimarika pakubwa.
Brazil wachezaji wake walikuwa wamecheza kwa wastani mechi
28.04 mwaka 2002, Italia 32.91 mwaka 2006 na Uhispania 38.30 mwaka 2010.
Mataifa matatu tuliyobaki nayo yalipotangaza wachezaji wake,
Ufaransa uzoefu wa wastani wachezaji wake ni mechi 24.56, Ujerumani 43.26 na
Ubelgiji 45.13.
Usiwe bingwa mtetezi
Kombe la Dunia huwa ngumu sana kutetea. Haijatokea tangu
Brazil walipofanikiwa kutetea taji hilo kwa kushinda 1958 na 1962 ambapo taifa
limeshinda mara mbili mfululizo.
Kusema kweli, tangu wakati huo wa Brazil, mabingwa watetezi
13 ambao wamekuwepo walipita nusu fainali mara mbili pekee.
Argentina mwaka 1990 na Brazil mwaka 1998, ingawa Brazil
walimaliza wa nne mwaka 1974 mpangilio ulipokuwa wa hatua mbili za makundi na
kisha fainali.
Katika michuano minne iliyopita, mabingwa watetezi
waliondolewa hatua ya makundi mara tatu.
Ujerumani wamefanikiwa sana Kombe la Dunia miaka ya
karibuni.
Katika michuano tisa iliyoandaliwa karibuni - ikiwemo mitatu
wakiwa Ujerumani magharibi - wameshinda mara mbili, wakafika fainali mara
nyingine tatu na wakamaliza nafasi ya tatu mara nyingine mbili.
Hata hivyo, ukiangalia uwezekano wao wa kushinda tena Urusi,
historia haipo nao.
Kwa hivyo, tuko hapo sasa. Ubelgiji watashinda Kombe la
Dunia. Taifa jingine lisiposhinda. Jambo ambalo linawezekana.
Comments
Post a Comment