- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
SERIKALI imetenga shilingi bilioni 700 kwa ajili ya
utekelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme wa Rufiji (Stieglers Gorge)
unaotarajiwa kukamilika Julai 2018.
Hayo yalibainishwa jijini hapa leo na Waziri wa Nishati,
Dkt. Medard Kalemani, wakati akiwasilisha bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi
ya wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2018/19 ambayo ni shilingi trilioni 1.69.
Waziri Kalemani alisema, mkandarasi ataanza kazi za awali
kwa miezi mitatu na kufuatiwa na ujenzi wa miundombinu ya mradi unaotarajiwa
kukamilika kwa kipindi cha miezi 36.
Alisema lengo la kutekeleza mradi huo ni kuzalisha umeme wa
jumla ya Megawati 2,100 kwa kutumia maji, katika Bonde la Mto Rufiji.
“Utekelezwaji wa mradi huu mkubwa nchini ni kichocheo muhimu
katika kuwezesha Tanzania kufikia azma yake ya kuwa nchi ya uchumi wa kati
ifikapo mwaka 2025,” alisema.
Aliongeza kuwa, katika kipindi cha mwaka 2017/18 hatua
iliyofikiwa ni pamoja na kufanya uchambuzi wa zabuni zilizowasilishwa na
wakandarasi walioonyesha nia ya kutekeleza mradi huo.
Aidha, ujenzi wa njia ya msongo wa kV 33 kutoka eneo la Dakawa
kwa ajili ya kupeleka umeme unaotumiwa na mkandarasi wakati wa ujenzi wa mradi
huo ulianza Novemba mwaka 2017 na unatarajiwa kukamilika Julai 2018.
“Katika kipindi cha mwaka 2017/18 serikali itaendelea
kutekeleza mradi huu ambapo kazi zitakazofanyika ni pamoja na ujenzi wa kambi
na ofisi za wafanyakazi, ujenzi wa bwawa na njia kuu za kupitisha maji,” alisema.
Aliongeza kuwa, utekelezaji wa shughuli za ujenzi huo
unatarajiwa kuanza Julai mwaka huu na kwamba tayari mkandarasi anakaribia
kuanza kazi ya awali.
Miradi mingine inayotarajiwa kutekelezwa ni pamoja na
upanuzi wa kituo cha kuzalisha umeme cha Kinyerezi 1 kwa kuongeza mitambo
itakayozalisha Megawati 185 na kukifanya kutoka uzalishaji wa Megawati 150
kuzalisha Megawati 335.
Alisema mradi huo unagharamiwa na serial kea asilimia 100
kea gharama ya takribani shilingi. bilioni 434 na kwamba katika mwaka wa fedha
2017/18 kazi zilizokamilika ni ujenzi wa misingi ya kusimika mitambo ya
kuzalisha umeme na transfoma.
Nyingine ni ujenzi wa kituo cha kupoza umeme, ujenzi wa njia
ya msongo wa kV 220 inayounganisha mtambo wa Kinyerezi 1 na 11 na kuunganishwa
katika gridi ya taifa.
Alisema katika kipindi cha mwaka 2018/19 kazi ya usimikaji
wa mitambo pamoja na ukamilishaji wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme
zitafanyika kwa gharama ya shilingi bilioni 164 ambazo ni fedha za ndani.
Comments
Post a Comment