- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Na
Mwandishi Wetu, MAELEZO
Kilimanjaro
WATANZANIA
wametakiwa kuendelea kumuunga mkono Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika kuleta
mageuzi makubwa ya kiuchumi nchini kwa kuhakikisha kuwa wanakuwa mstari wa
mbele katika kulipa kodi ili kuiwekeza Serikali kutekeleza miradi mikubwa ya
maendeleo.
Hayo
yamesemwa jana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dkt. Hassan Abbasi
wakati wa mahojiano ya kipindi maalum na Redio Boma FM Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro
na kuwataka wananchi kuiachia Serikali yao iwatendee haki ya kikatiba katika
kuwaletea maendeleo yaliyokusudiwa.
Dkt.
Abbasi alisema Watanzania kwa sasa wamepata Serikali makini na sikivu inayowajibika
kwa wananchi wake kwa kuwa imeweza kuelewa matatizo na kero mbalimbali za muda
mrefu zilizokuwa zikiwakabili katika jitihada zao za kujieletea maendeleo.
Alisema
tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza ya Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius
Nyerere kumekuwa na shabaha mbalimbali zilizowekwa ikiwemo malengo ya kuwa na
nchi ya uchumi wa viwanda ambayo hata hivyo ilishindwa kufikiwa lakini kwa sasa
imefanikiwa katika Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John
Pombe Magufuli.
Aliongeza
kuwa yapo maendeleo makubwa yanayoendelea kufanyika katika sekta zote za
maendeleo nchini hususani kupitia miradi mikubwa inayogusa maisha ya kila siku
ya wananchi ikiwemo nishati, maji, elimu, afya na kadhalika ambapo tayari
mageuzi yake yameanza kuleta matokeo chanya kwa Watanzania walio wengi.
“Kwa
kipindi kirefu tumekuwa na kilio cha umeme wa uhakika hususani kwa wananchi wa
vijijini, lakini tunapozungumza kwa sasa Serikali inatekeleza miradi mikubwa ya
umeme ikiwemo Kinyerezi I na kuongeza upanuzi wa megawati kutoka Megawati 150
hadi 185, ni umeme mkubwa unaoweza kulisha mikoa mingi zaidi” alisema Dkt. Abbasi.
Akiendelea
kugusia sekta ya nishati, Dkt. Abbasi alisema Serikali pia imeanza maandalizi
ya mradi wa umeme wa Stieglers Gorges ambao ni mradi wa kihistoria uliopangwa
kutekelezwa na Hayati Baba wa Taifa na kushindwa kufanyika ambapo hata hivyo
Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi chake cha utawala wa miaka mitatu
tayari imetangaza zabuni ya ujenzi wa mradi huo unaotarajia kuzalisha megawati
2500.
Aidha
Dkt. Abbasi anasema Serikali ya Awamu ya Tano pia inatekeleza miradi mikubwa ya
maji katika Mikoa na Halmashauri mbalimbali nchini katika kasi ya kuridhisha
ambapo wakandarasi wake wanaendelea kusimamiwa kwa karibu zaidi na Serikali ili
kuifanya kazi hiyo kwa ubora na viwango vilivyopo katika mikataba ya zabuni.
Kuhusu
Viwanda, Dkt. Abbasi anasema Serikali ya Awamu ya Tano imekusudia kuwa na nchi
ya Uchumi wa Viwanda, ambapo hadi sasa kuna zaidi ya viwanda 3000
vilivyoanzishwa chini ya Utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano, juhudi
zinazolengwa kutengeneza ajira nyingi zaidi kwa Watanzania.
Aliongeza
kuwa ili kufanikisha adhma ya kufikia uchumi wa Viwanda, Serikali imechukua
hatua mbalimbali katika kuboresha na kuimarisha sekta ya usafirishaji nchini
ikiwemo usafiri wa anga na majini kwa kununua ndege na meli kubwa zitakazoweza
kusafirisha bidhaa mbalimbali ndani na nje ya nchi.
“Serikali
imekamilisha meli mbili za MV Ruvuma na MV Njombe ambazo ni meli za mizigo
zitakazokuwa zikisafirisha mizigo baina ya Tanzania na Malawi sambamba na
kuboresha na kukarabati Meli ya MV Glorias ambazo tayari zimeanza kufanya kazi
katika Ziwa Tanganyika sambamba na miradi mingine mikubwa ya Maendeleo” alisema
Dkt. Abbasi.
Comments
Post a Comment