- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Na
Mwandishi Wetu, MAELEZO
Kilimanjaro
UFAHAMU
wa shida na kero za Watanzania, nidhamu ya matumizi ya fedha za umma na mfumo
imara wa ufuatiliaji wa miradi ya maendeleo vinaelezwa kuwa ndiyo siri kubwa ya
mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe
Magufuli.
Hayo
yamesemwa jana Mkoani Kilimanjaro na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) na
Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbasi wakati wa mahojiano ya kipindi
maalum na Redio Boma FM, akizungumzia kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa miradi
mikubwa ya maendeleo iliyofikiwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya
Awamu ya Tano.
Dkt.
Abbasi alisema katika kipindi cha Utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano, Rais
Dkt. John Pombe Magufuli amekuwa mfano katika kusimamia utekelezaji wa maagizo
na maelekezo mbalimbali anayoyatoa kwa Watendaji Serikalini, hatua inayosadia
kujenga dhana ya nidhamu na uwajibikaji katika kuyafikia maendeleo ya wananchi.
“Rais
Magufuli katika kipindi cha miaka yake mitatu ya utawala ameweza kuishi katika
dhana ya kutenda na kufuatilia, mfano mzuri ni suala la kuhamia Dodoma ambapo
leo hii Viongozi wote wakuu wa Serikali wapo huko” alisema Dkt. Abbasi.
Aidha
Dkt. Abbasi alisema ipo mifano mbalimbali inayoakisi azma ya Rais Magufuli ya
kutaka kuleta maendeleo ya kweli kwa Watanzania ikiwemo ujenzi wa uchumi imara
ambapo hadi sasa ipo miradi mbalimbali ya maendeleio inayoendelea kutekelezwa
nchini ikiwemo ongezeko la ujenzi wa viwanda ambavyo vimeweza kuzalisha ajira
kubwa kwa Watanzania.
Akifafanua
zaidi Dkt. Abbasi alisema ni wajibu wa Watendaji wote Serikalini kusimamia na
kuyasemea mafanikio hayo katika maeneo yao ya kazi, kwani kwa kufanya hivyo
kutasaidia kutoa ufafanuzi wa hoja na masuala mbalimbali ambayo yamekuwa
yakipotoshwa kwa makusudi na baadhi ya watu katika jamii.
Aidha
aliwataka Maafisa Habari na Mawasiliano Serilalini kujenga mazoea ya kutumia
majukwaa mbalimbali ikiwemo mitandao ya kijamii ili kuweza kuisemea Serikali katika
kwa kujibu hoja mbalimbali zinazoelezwa katika maeneo yao ya kazi kwani kwa
kufanya hivyo wataweza kuisaidia Serikali kwa kutoa ufafanuzi katika upotoshaji
unaofanywa na watu wachache.
Dkt.
Abbasi alisema Serikali ya Awamu ya Tano kamwe haikatishwi tamaa na wakosoaji
wa maendeleo, na badala yake inaendelea kufanya kazi kwa kasi na itahakikisha kuwa
itaendelea kuonyesha na kutangaza mafanikio ya miradi mikubwa ya maendeleo
iliyotekelezwa na Serikali katika maeneo mbalimbali nchini.
“Hata
maendeleo ya miji mikubwa duniani ikiwemo Beijing, New York na London watu wake walifanya kazi kubwa sana na Sisi
katika Serikali ya Awamu ya Tano tunaahidi na tuatekeleza kwa kupigania maisha
ya Watanzania ili kufikia malengo tuliyojiwekea” alisema Dkt. Abbasi.
Comments
Post a Comment