- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
JAMHURI
YA MUUNGANO WA TANZANIA
BARAZA
LA MICHEZO LA TAIFA (BMT)
Simu: +255
(222) 2850015 Barabara
ya Taifa,
Baruapepe: info@nationalsportscouncil.go.tz Uwanja
wa Taifa,
Tovuti: www.nationalsportscouncil.go.tz Ghorofa
ya 2,
S.L.P
20116,
DAR ES SALAAM.
8 Februari,
2018
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
UTARATIBU
WA KUWASILISHA MALALAMIKO AU RUFAA KATIKA SEKTA YA MICHEZO NCHINI
Shughuli za Michezo nchini zinafanyika kwa mujibu wa
sheria ya Baraza la Michezo la Taifa namba 12 ya mwaka 1967 na marekebisho yake
ya sheria namba 6 ya mwaka 1971.
Aidha, kutokana na kufanyika kwa shughuli mbalimbali, kila chama, shirikisho,
klabu au asasi na taasisi zina miongozo mbalimbali inayosaidia kuendesha
michezo katika maeneo yao.
Hata hivyo, katika kutekeleza shughuli za michezo kama
vile mashindano, yamekuwa yakiibuka malalamiko/migogoro ambayo kwa namna moja
au nyingine inahitaji utatuzi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu stahiki
hasa kwa vyama vilivyosajiliwa kama vile:-
(a)
Vyama vya
Michezo;
(b)
Mashirikisho
ya Michezo;
(c)
Vilabu vya
Michezo;
(d)
Taasisi za
Kimichezo
(e)
Wadau wote
wa michezo nchini.
Ieleweke kuwa, ziko taratibu za kufuata katika
kuwasilisha malalamiko/migogoro kama ifuatavyo:
1)
Malalamiko/rufaa
ya Mchezaji, Kiongozi, Chama, Klabu, Mwalimu, Mwamuzi, Daktari wa Timu au mdau mwingine wa michezo anao uhuru na
haki ya kuwasilisha malalamiko yake/rufaa kwa kufuata utaratibu kwa ngazi ya
juu endapo hakuridhika na uamuzi uliotolewa na Uongozi wa Ngazi husika kama
vile;
a) Katika ngazi ya Wilaya:
i)
Malalamiko
yatapelekwa kwa Chama cha Mchezo husika na kwa mujibu wa Kanuni za mchezo
husika. Nakala yake itapelekwa katika
Kamati ya Michezo ya Wilaya katika muda usiozidi siku tatu (3) baada ya uamuzi
kutolewa;
ii)
Kama
mlalamikaji hataridhika atakata rufaa kwa Kamati ya Nidhamu, Rufaa na
Usuluhishi ngazi ya Wilaya katika muda usiozidi siku saba (7). Nakala yake itapelekwa ngazi ya michezo ya
Mkoa na Kamati ya Michezo ya Mkoa;
iii)
Kama mlalamikaji
hataridhika na uamuzi wa Kamati ya Michezo ya Wilaya atakata rufaa kwa Kamati
ya Michezo ya Mkoa katika muda usiozidi siku saba (7) na nakala itapelekwa
Baraza la Michezo na Chama cha Mchezo ngazi ya Taifa;
iv)
Endapo
hataridhika na Uamuzi wa Baraza atakuwa na haki ya kukata rufaa kwa Waziri
katika muda wa siku saba (7) na maamuzi ya Waziri yatakuwa ya mwisho.
b) Katika
Ngazi Mkoa.
i)
Mlalamikaji
atakata rufaa kwa Chama cha Michezo ngazi ya Mkoa katika muda usiozidi siku
tatu (3) na nakala itapelekwa kwenye Kamati ya Michezo ya Mkoa;
ii)
Kama
hajaridhika na maamuzi ya Chama cha Michezo ngazi ya Mkoa atakata rufaa kwa
Kamati ya Michezo ya Mkoa katika muda usiozidi siku saba (7) nakala yake
itapelekwa kwa Chama cha Mchezo cha Taifa na Baraza la Michezo la Taifa. Kamati ya Michezo ya Mkoa itahakikisha upo
ujumbe wa Chama ngazi ya Mkoa rufaa hiyo itakaposikilizwa;
iii)
Kama
mlalamikaji hataridhika, atakata rufaa kwa Baraza la Michezo la Taifa katika
muda usiozidi siku saba (7). Baraza la
Michezo la Taifa lihakikishe kuna ujumbe wa Chama ngazi ya Taifa linapojadili
rufaa hiyo;
iv)
Endapo
mlalamikaji hataridhika na uamuzi wa Baraza la Michezo atakuwa na haki ya
kukata rufaa kwa Waziri wa Michezo katika siku saba (7) na maamuzi ya Waziri
yatakuwa ni ya mwisho.
c)
Ngazi ya Taifa:
i)
Mlalamikaji
atakata rufaa kwa Baraza la Michezo la Taifa katika muda usiozidi siku saba (7)
nakala itapelekwa kwa Waziri;
ii)
Asiporidhika
na uamuzi wa Baraza atakata rufaa kwa Waziri katika muda usiozidi siku saba (7)
na uamuzi wa Waziri utakuwa ni wa mwisho.
Hivyo Basi, kwa utaratibu huu, Vyama vyote, mashirikisho
na Vilabu na Wadau wa Michezo nchini, mnasisitizwa kufuata utaratibu huu ambao
ni muhimu ili kutoruka ngazi ili kupata maamuzi na ushauri stahiki kwa manufaa
ya maendeleo ya Michezo, ustawi wa jamii na Taifa kwa ujumla katika kuimarisha Utawala
Bora.
Imetolewa na:
Frank Mgunga,
Afisa Habari.
Comments
Post a Comment