Featured Post

BALOZI WA IRELAND NCHINI TANZANIA, INDONESIA NA MWAKILISHI WA UNFPA WAMUAHIDI USHIRIKIANO RC MTAKA

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kushoto) akimkabidhi Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Prof Ratlan Pardede Mwongozo wa uwekezaji Mkoa wa Simiyu.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kulia) akifurahia jambo na Muwakilishi Mkaazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi Jacqurline Mahon.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka (Kulia) akisalimiana na Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock ofisini kwake Jijini Dar es salaam.

Na Mathias Canal, Wazo Huru Blog

Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock amemuahidi Mkuu wa Mkoa wa simiyu Mhe Antony Mtaka kuendeleza ushirikiano na Mkoa wa Simiyu ili kuboresha sekta ya Afya kupitia Irish Aid.

Balozi huyo ameyasema hayo wakati wa mazungumzo ya pamoja na Mhe Mtaka ambapo tayari kwa pamoja wamekubaliana kuanza kutekelezwa wa kusudio hilo tarehe 6 Februari 2018 kwa kuanza na timu ya wataalamu kufika Mkoani humo ili kuanza haraka shughuli hiyo.

Balozi H.E Ambassador Paul Sherlock amemuahidi Mhe Mtaka kuwa tayari nchi yake ya Ireland imekusudia kwa dhati kushirikiana vyema na Mkoa huo huku akisisitiza kuendelea kushirikiana zaidi pia katika utekelezaji wa miradi ya Maendeleo kwenye sekta ya Mifugo, Kilimo na Utalii.

Balozi wa Ireland nchini Tanzania H.E Ambassador Paul Sherlock ametoa kauli hiyo ya kuunga mkono juhudi za Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka za kutoka kuboresha sekta mbalimbali ikiwemo uwekezaji wakati alipokutana na kufanya mazungumzo leo 2 Februari 2018 katika.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe Antony Mtaka amemshukuru Balozi Sherlock kwa ubalozi wa Ireland kukubali kuwezesha safari ya mafunzo kwa wataalamu wawili kutoka Mkoani Simiyu kwenda nchini Ireland kuanzia Februari 12 mpaka 16 Machi 2018 kwa ajili ya kupata mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) hasa kwenye upande wa uhifadhi wa Data za Mkoa.

Katika hatua nyingine Mkuu huyo wa Mkoa wa Simiyu Mhe Mtaka alikutana na kufanya mazungumzo na Muwakilishi Mkaazi wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na Idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi Jacqurline Mahon ambapo pamoja na mambo mengine Shirika hilo limetoa zaidi Bilioni 3 kwa ajili ya kukarabati vituo vya afya  na upasuaji ndani ya Halmashauri zote za Mkoa wa Simiyu.

Pia UNFPA imeahidi kutoa magari kwa Halmashauri 6 za Mkoa wa Simiyu kwa ajili ya kuboresha huduma za afya, ambapo tayari UNFPA wameamua kujenga ofisi yao ndogo ndani ya Mkoa wa Simiyu itakayoratibu shughuli mbalimbali za shirika hilo kwa mikoa yote ya kanda ya ziwa.

Wakati huo huo Mhe Mtaka amekutana na Balozi wa Indonesia nchini Tanzania Prof Ratlan Pardede ambaye  pamoja na mambo mengine amekubali kutembelea Mkoa wa Simiyu mwezi Macih mwaka huu 2018 huku akiwaalika wataalamu wa Mkoa wa Simiyu nchini Indonesia mwezi Aprili mwaka huu.

Aidha, Balozi huyo Prof Pardede alisema kuwa pia sekta rasmi ya Indonesia itazuru Mkoani Simiyu ili kuona uwezekano wa kujenga kiwanda kitakachosaidia kuongeza thamani ya zao la pamba, kuboresha mkoa dada wa Indonesia na Simiyu katika mazao ya Mpunga na pamba pamoja na kualika wawekezaji wa Indonesia kuwekeza Mkoani Simiyu kwa kuzingatia Mwongozo wa uwekezaji wa Mkoa wa Mkoa huo (Simiyu Investment Guide) ambao ameusifia kwamba ni wa kipekee na alipouona mwongozo huo kupitia mtandao wa Youtube aliona ukiwa umeitangaza sana Tanzania na wafanyabiashara wa Indonesia walihamasika sana kuuona na kuusoma katika Tovuti hiyo.

Comments