Featured Post

MHE MWANJELWA AWATAKA WANANCHI MBEYA KUUNGA MKONO JUHUDI ZA RAIS MAGUFULI KWA VITENDO

Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akiwasihi waumini kumuunga mkono na kumuombea Rais Magufuli wakati akitoa salamu kwenye ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akimlisha chakula mmoja ya wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa pamoja na Viongozi wengine wakiongoza maombi wakati wa ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.
 Miongoni mwa wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.
 Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akifanyiwa maombi na viongozi wa dini wakati wa ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.
Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa akishiriki chakula cha mchana na wazee waliohudhuria ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya, Leo 1 Januari 2018.

Na Mathias Canal, Mbeya

Wananchi Mkoani Mbeya wametakiwa kuunga mkono kwa vitendo juhudi za uwajibikaji wa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli.

Mwito huo umetolewa Leo 1 Januari 2018 na Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo Mhe Dkt Mary Mwanjelwa wakati akitoa salamu kwenye ibada ya Siku ya Wazee iliyofanyika katika kanisa La Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) lililopo Katika Mtaa wa Sinde B, Kata ya Manga Jijini Mbeya.

Alisema kuwa Rais Magufuli na serikali anayoingoza anawathamini kwa kiasi kikubwa wazee kote nchini kwani kwa umri wao ni sehemu ya turufu muhimu kimawazo na busara katika utendaji ndio maana Mke wake Mhe Mama Janeth Magufuli hushirikiana na wazee waliopo katika makundi mbalimbali katika huduma za kijamii.

Alisema kuwa serikali hii ya awamu ya Tano inayochagizwa na kauli mbiu isemayo "HAPA KAZI TU" inawakumbusha na kuwahamasisha wananchi kufanya kazi kwa bidii ili kuinua haraka uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Katika ibada Hiyo Mhe Mwanjelwa ameshiriki chakula cha mchana na wazee waliohudhuria ibada Hiyo ya siku ya wazee kutoka Kata ya Manga na Sinde ikiwa ni ishara ya mapokezi mema ya Mwaka Mpya 2018. 

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Wizara ya Kilimo aliongoza waumini wa kanisa la Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) kumuombea Rais Magufuli sambamba na serikali kwa ujumla ili wananchi waendelea kujivunia matunda ya Rais Magufuli ambaye Duniani kote anasifika kwa umakini na ushupavu.

Alisema kuwa zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu kwa kanisa hilo kushirikiana kwa Karibu na wazee huku akisema kuwa litakuwa jambo zuri na muhimu zaidi endapo litafanyika kwa ajili ya wazee wa Mkoa mzima wa Mbeya.

"Wazee ni Tunu, kuwa Mzee ni Baraka kwani hata vijana ni wazee wajao, Lakini niwasihi kuendelea kuwatumia wazee kwa ushauri wa kijamii pia kidini lakini zaidi Mwaka Mpya 2018 uwe Mwaka wa Mafanikio kwetu sote:" Alikaririwa Mhe Mwanjelwa

Mhe Mwanjelwa Alisifu uongozi wa kanisa hilo kwa kumualika kushiriki nao katika ibada hiyo huku akiwapongeza kwa kufanya ibada ya kiroho lakini pia ibada ya kimwili kwa ushirikishaji wa jamii.

Naye Kiongozi Mkuu wa Kanisa la Huduma ya Maombezi na Uponyaji (Jesus Healing Centre T. Ministry) Mchungaji Capson Masimbani alimpongeza Mhe Mwanjelwa na kusema kuwa ni kiongozi mwenye kujali wananchi pasina kubagua itikadi za dini zao.

Alisema kuwa ni Viongozi wachache nchini ambao wana unyenyekevu kama yeye huku akimsihi kuendelea na busara na hekima Hiyo.

Sambamba na hayo Mhe Naibu Waziri wa Kilimo aliunga mkono juhudi za kanisa hilo kwa kuandaa sherehe hiyo ya siku ya wazee kwa kuwapatia mifuko 66 ya sukari wazee hao.

Comments