Featured Post

KAIMU MKURUGENZI UZALISHAJI MIFUGO NA MASOKO WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI DK. ASSIMWE RWIGUZA ASHIRIKI UPIGAJI CHAPA MIFUGO KATIKA MKOA WA SHINYANGA

 Kaimu Mkurugenzi wa uzalishaji  Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,  Dk. Assimwe Rwiguza akipigaji chapa ng’ombe katika Kijiji cha Idodoma Wilaya ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya timu ya wataalamu 15 wa mifugo walioko katika mikoa 26 kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa zoezi la upigaji chapa linalotarajiwa kukamilika January 31 mwaka huu.
 Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Dk  Asimwe  Rwiguza akitoa ufafanuzi wa mahali sahihi panapotakiwa kupiga chapa kwa ng'ombe kwa wafugaji wa Kijiji cha Idodomya wilayani Shinyanga. kushoto ni Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya Shinyanga, Dk. Clement Batisiliko
Kaimu Mkurugenzi wa Uzalishaji Mifugo na Masoko wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi  Dk.  Asimwe  Rwiguza akitoa ufafanuzi kwa wafugaji wa Kijiji cha Idomya umuhimu wa kupiga chapa mifugo yao kabla ya muda wa nyongeza uliowekwa na Serikali kumalizika wa Januari 31 mwaka huu ambapo Dk. Assimwe ni miongoni mwa timu ya wataalamu 15 wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi walioko kwenye mikoa 26 ya Tanzania bara kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa zoezi la upigaji chapa.

Comments