Featured Post

MAGONJWA YA SUNGURA: KUVIMBA MACHO NA UGONJWA WA MIFUPA KUZUNGUKA MACHO (EXOPHTHALMOS)


Na Daniel Mbega, MaendeleoVijijini Blog

WAFUGAJI wa sungura wanaweza kuwa wameshuhudia wakati mwingine macho ya sungura wao yakionekana kutokeza juu zaidi au kuwa pembeni na kushindwa kuzunguka kama ilivyo kawaida.
Tatizo hili kitaalam linaitwa Exophthalmos ambapo macho ya sungura huwa yako pembeni ya mfumo wake kutokana na ugonjwa au uvimbe nyuma ya jicho.

Jicho linakuwa limesukumwa kwa mbele na nje ya soketi yake, lakini inategemea na mahali uvimbe ulipo, kwani jicho pia linaweza kusukumwa hata kwa nyuma ikiwa uvimbe uko mbele.
Sungura wako, hasa wa jamii ya Dwarf na Lop, pamoja na wale wa kawaida walio katika umri wa kati wanaweza kupatwa na tatizo hili kutokana na matatizo ya msingi ya meno au ya kinywa.

Dalili na Aina

Aina za magonjwa haya ya njia ya mzunguko wa macho (orbital disease) ni pamoja na:
* Jicho kukaa pembeni (malpositioned eye) — husababishwa na mabadiliko ya ukubwa (kupungua au kuongezeka) kwa vitu kwenye jicho, au kuvimba kwa misuli ya juu ya jicho (extraocular muscle)
* Kuvimba kwa jicho (Enophthalmos) — husababishwa na kukosekana kwa ukubwa wa nafasi ya kuzunguka kwa jicho au nafasi hiyo kuvimba kwa juu na kulisogeza jicho mbele
* Makengeza (Strabismus) — mzunguko usio wa kawaida wa macho – husababishwa na mwenendo mbovu wa misuli.
Dalili za matatizo haya ya mzunguko wa macho zinaweza kutofautiana lakini zinahusisha magonjwa ya meno, kurefuka kwa meno aina ya machonge (incisors), kutokwa majimaji puani, na maambukizi katika mfumo wa juu wa upumuaji.
Dalili nyingine ni:
* Uchovu na kukosa nguvu
* Taharuki
* Kuvimba au kushuka kwa kigubiko cha jicho
* Kusaga meno
* Kunywa sana maji
* Kudondosha hovyo chakula wakati wa kutafuna
* Muonekano usio pacha, hususan sungura kuwa na tungamo pamoja na usaha wa mizizi ya meno
* Mabadiliko ya tabia katika unywaji na ulaji (kama, kupendelea vyakula laini)
* Kukaa kwa kubinuka na kutopenda kusogea.

Uchunguzi

Daktari wa mifugo anaweza kufanya uchunguzi kwa sungura kujua tatizo ni nini. Uchunguzi wa njia ya X-Ray kwenye kichwa unaweza kufanyika pamoja na kupiga X-Ray kwenye kifua ili kuona matatizo katika njia ya upumuaji.
Uchunguzi katika njia ya mzunguko wa macho (orbital ultrasonography) unaweza pia kufanyika ili kutoa taswira halisi ya uvimbe ulivyo, na kipimo cha Computed Tomography (CT scan) kinaweza kutumia kutazama eneo zima la kuzunguka macho. 
Uchunguzi wa mdomo na pua unafanyika pia kwa kutumia sampuli ya majimaji inayoweza kuchukuliwa kwa sindano kutoka kwenye njia ya mzunguko wa macho.
Kama kutakuwa na tungamo kwenye njia ya mzunguko wa macho, kipimo cha biopsy kinaweza kutumika ili kuona kama kuna kansa.

Tiba

Tiba itagemea na sababu za tatizo husika na matokeo ya uchunguzi wa mwisho. Kama kutakuwa na utando wa ziada wa mafuta nyuma ya macho, kwa mfano, kupunguza uzito ni jambo linaloshauriwa.
Lakini sungura atapatiwa dawa za antibiotics kuondoa maambukizi ya bacteria.
Kama maambukizi yamesababisha kuwepo kwa usaha, basi upasuaji utahitaji ambao baadaye utahitaji dawa za kupunguza maumivu pamoja na jeli maalum za kupaka katika eneo la kuzunguka jicho.

Matunzo  

Katika kipindi chhote cha matibabu sungura wako aendelee kula vizuri, tena vyakula laini ambavyo ataweza kutafuna mpaka atakapokuwa na uwezo wa kutafuna vyakula vigumu.
Utaendelea kumpa sungura wako vyakula maalum vya punje na kumhamasisha kula.

Imeandaliwa na www.maendeleovijijini.blogspot.com. Tupigie: +255 656 331974


Comments