Featured Post

MWIGULU AFUNGUA MKUTANO WA WADAU WA WAKIMBIZI

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wakimbizi   na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Makamu Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Volker Turk, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika hilo. Majadiliano hayo yamehusu   masuala ya uhifadhi wa   wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi   walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mwakilishi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) nchini Tanzania, Chansa Kapaya, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika hilo .Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wa wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi   walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kushoto ni Makamu Kamishna Mkuu wa Shirika hilo, Volker Turk .Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahaya, akizungumza wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya  uhifadhi wa wakimbizi   na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 

Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Marijani,   akichangia hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika hilo. Majadiliano hayo yamehusu masuala ya  uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi   walioko katika Kambi mbalimbali nchini..Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mratibu wa Mpango wa Kuwahudumia wakimbizi  ,Dkt. John Jingu, akizungumza wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya wakimbizi   na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko katika Kambi mbalimbali nchini. Kushoto ni Mkurugenzi wa CSFM, Prof. Bonaventure Rutinwa. Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (wanne kulia waliokaa), Makamu Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Volker Turk(watano kulia waliokaa), wakiwa katika picha ya pamoja na washriki wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya  uhifadhi wakimbizi   na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.

Na Mwandishi Wetu
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amefungua Kikao kinachowakutanisha Wadau wa Masuala ya Wakimbizi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Watendaji Wakuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), leo jijini Dar es Salaaam.
Akizungumza wakati wa Ufunguzi huo, Mwigulu aliwataka washiriki wa kikao hicho kujadili kwa kina na kufikia makubaliano juu ya suala la uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi huku akiahidi Serikali iko tayari kupokea wakimbizi kama ilivyokuwa desturi   huku akisisitiza Serikali haitumvumilia mkimbizi atakaevunja sheria na kuwaasa kufanya utaratibu wa kurudi katika nchi zao wakimbizi ambao nchi zao hali ya usalama imerejea.
Tukiwa leo tuko katika kikao hiki cha viongozi wa juu wa Serikali na Uongozi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi, nina imani tutafikia muafaka juu ya suala la uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi, Serikali ya Tanzania imekua na desturi ya muda mrefu ya kupokea wakimbizi na kuwahudumia,ila nawaaasa wadau wote washirikiane kwa pamoja katika kubeba gharama  zinazohusu  jambo la kuwahifadhi wakimbizi,” alisema Mwigulu
Akizungumza wakati wa Kikao hicho, Makamu Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Volker Turk, alisema wamekuja nchini ili kujadili suala nzima la uhifadhi wakimbizi na kupokea maoni kutoka kwa nchi wenyeji huku akisisitiza lengo la kikao hicho ni kuona jinsi gani changamoto mbalimbali zinazoletwa na wakimbizi zinaweza kutatuliwa.
“Napenda kwanza kuishukuru Serikali ya Tanzania na wananchi wanaoishi katika jamii zilipo kambi za wakimbizi kwa ukarimu wao wa muda mrefu wa kuwapokea wakimbizi kutoka nchi mbalimbali wanaokimbia machafuko katika nchi zao,tunafahamu changamoto wanazopata jamii hizo, ndio maana tumeomba kukutana na Serikali kuona suluhisho la kudumu la changamoto hizo.
Kikao hicho kimewashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Mambo ya Nje,Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali,Ofisi ya Rais,Wakuu wa Mikoa zilipo kambi za wakimbizi na Viongozi wa juu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani kutoka Makao Makuu nchini Geneva.


Comments