- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Unknown
on
- Get link
- Other Apps
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, akizungumza wakati wa Ufunguzi wa
Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia
Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wakimbizi
na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko
katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es
Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Makamu
Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Volker Turk,
akichangia hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya
Serikali na Shirika hilo. Majadiliano hayo yamehusu masuala
ya uhifadhi wa wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko
katika Kambi mbalimbali nchini.Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu
Nchemba.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi
Mwakilishi
wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) nchini Tanzania, Chansa
Kapaya, akichangia hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya
Serikali na Shirika hilo .Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wa wakimbizi
na suluhisho la kudumu la wakimbizi
walioko katika Kambi mbalimbali nchini.Kushoto ni Makamu Kamishna Mkuu
wa Shirika hilo, Volker Turk .Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es
Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Balozi Hassan Simba Yahaya, akizungumza
wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la
Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wa wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko
katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es
Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Kamishna
wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Nsato Marijani, akichangia
hoja wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na
Shirika hilo. Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la
wakimbizi walioko katika Kambi
mbalimbali nchini..Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es Salaam.Picha na
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Mratibu
wa Mpango wa Kuwahudumia wakimbizi ,Dkt.
John Jingu, akizungumza wakati wa Kikao cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya
Serikali na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo
yamehusu masuala ya wakimbizi na
suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko katika Kambi mbalimbali nchini. Kushoto
ni Mkurugenzi wa CSFM, Prof. Bonaventure Rutinwa. Kikao hicho kimefanyika leo, jijini
Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba (wanne kulia waliokaa), Makamu
Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), Volker
Turk(watano kulia waliokaa), wakiwa katika picha ya pamoja na washriki wa Kikao
cha Majadiliano ya Ngazi za Juu kati ya Serikali na Shirika la Kuhudumia
Wakimbizi Duniani (UNHCR).Majadiliano hayo yamehusu masuala ya uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi walioko
katika Kambi mbalimbali nchini.Kikao hicho kimefanyika leo, jijini Dar es
Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
IMEANDALIWA
NA KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI-WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI.
Na Mwandishi Wetu
Waziri
wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, amefungua Kikao kinachowakutanisha
Wadau wa Masuala ya Wakimbizi kutoka Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Watendaji Wakuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR), leo
jijini Dar es Salaaam.
Akizungumza
wakati wa Ufunguzi huo, Mwigulu aliwataka washiriki wa kikao hicho kujadili kwa
kina na kufikia makubaliano juu ya suala la uhifadhi wakimbizi na suluhisho la
kudumu la wakimbizi huku akiahidi Serikali iko tayari kupokea wakimbizi kama
ilivyokuwa desturi huku akisisitiza Serikali haitumvumilia
mkimbizi atakaevunja sheria na kuwaasa kufanya utaratibu wa kurudi katika nchi
zao wakimbizi ambao nchi zao hali ya usalama imerejea.
“Tukiwa leo tuko katika kikao hiki cha viongozi wa juu wa
Serikali na Uongozi wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi, nina imani tutafikia
muafaka juu ya suala la uhifadhi wakimbizi na suluhisho la kudumu la wakimbizi,
Serikali ya Tanzania imekua na desturi ya muda mrefu ya kupokea wakimbizi na
kuwahudumia,ila nawaaasa wadau wote washirikiane kwa pamoja katika kubeba
gharama zinazohusu jambo la kuwahifadhi wakimbizi,” alisema
Mwigulu
Akizungumza
wakati wa Kikao hicho, Makamu Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi
Duniani (UNHCR), Volker Turk, alisema wamekuja nchini ili kujadili suala nzima
la uhifadhi wakimbizi na kupokea maoni kutoka kwa nchi wenyeji huku akisisitiza
lengo la kikao hicho ni kuona jinsi gani changamoto mbalimbali zinazoletwa na
wakimbizi zinaweza kutatuliwa.
“Napenda
kwanza kuishukuru Serikali ya Tanzania na wananchi wanaoishi katika jamii
zilipo kambi za wakimbizi kwa ukarimu wao wa muda mrefu wa kuwapokea wakimbizi
kutoka nchi mbalimbali wanaokimbia machafuko katika nchi zao,tunafahamu
changamoto wanazopata jamii hizo, ndio maana tumeomba kukutana na Serikali
kuona suluhisho la kudumu la changamoto hizo.
Kikao
hicho kimewashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo Serikali kupitia Wizara ya
Mambo ya Ndani ya Nchi, Wizara ya Mambo ya Nje,Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali,Ofisi ya Rais,Wakuu wa Mikoa zilipo kambi za wakimbizi na Viongozi wa
juu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani kutoka Makao Makuu nchini Geneva.
Comments
Post a Comment