- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Unknown
on
- Get link
- Other Apps
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Mbunge wa Mtama, Mhe. Nape Nnauye.
Makamu wa Rais amewasili mkoani Lindi tayari kwa kuhudhuria kilele cha sherehe za siku ya Wakulima (Nane Nane) ambapo kitaifa zinaadhimishwa mkoani Lindi.
Katika Uwanja wa ndege wa kikwetu Lindi, Makamu wa Rais pia alipokelewa na Viongozi wa Chama na Serikali pamoja na Vikundi vya ngoma ambavyo vilimlaki kwa nyimbo mbali mbali.
Kesho siku ya Kilele cha sikukuu ya Wakulima (Nane Nane), Makamu wa Rais atapata fursa ya kutembelea mabanda yakiwemo ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi katika maonesho hayo kwenye viwanja vya Ngongo kisha kuhitimisha kwa kuhutubia Wananchi kwenye maonesho hayo.
Comments
Post a Comment