- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Na Daniel Mbega, MaendeleoVijijini
IJUMAA Mei
6, 2011 Mbunge wa Mbeya Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema), Joseph Osmund Mbilinyi a.k.a Sugu, alitoa kauli yenye kuhamasisha
vurugu na machafuko wakati alipoanzisha ‘Operesheni Piga Mawe Mafisadi’, huku
akiwataka wafuasi wa Chadema kumpiga mawe Edward Lowassa kwa kuwa ni miongoni
mwa mafisadi hao, MaendeleoVijijini
inaripoti.
Kauli hiyo
ambayo Sugu aliitoa mbele ya maelfu ya wananchi na viongozi wakuu wa chama
hicho akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe na Katibu Mkuu wa wakati huo, Dk.
Wilbrod Slaa, katika viwanja vya Kibonde Nyasi, maarufu kama CCM Ilomba, jijini
Mbeya.
Akitumia muda
wa dakika 7 na sekunde 39, Sugu aliwataka wafuasi wa Chadema na wananchi
kuwapiga mawe viongozi wote wa CCM na Serikali ambao walitajwa kwenye ufisadi,
huku akisema zama za vijana maskini kuuana wenyewe kwa wenyewe kwa kuibiana
simu na cheni zimekwisha na sasa ilikuwa zamu ya kuwapiga mawe viongozi wote
waliotajwa kuwa mafisadi ambao ndiyo sababu ya hali ngumu ya maisha.
Tayari Lowassa,
ambaye aliitwa fisadi na kuhubiriwa nchi nzima na viongozi wote wa Chadema kwa
miaka takriban saba, yupo na chama hicho na katika hatua ya kushangaza, ndiye
waliyemteua kuwa mgombea urais wa chama pamoja na mwamvuli wa Umoja wa Katiba
ya Wananchi (Ukawa) mwaka 2015.
MaendeleoVijijini inafahamu kwamba, hakuna
kiongozi yeyote wa Chadema aliyewahi kuthubutu kutengua kauli hiyo ya Sugu
ambayo ilionyesha mtazamo hasi kisiasa na kijamii kwa kuwa ingeweza kuleta
vurugu na machafuko na hivyo kuchafua amani nchini.
MaendeleoVijijini inakuletea neno
kwa neno la hotuba hiyo ya Sugu, ambaye alikaribishwa na Benson Kigaila
aliyekuwa muongoza shughuli (MC):
Salaam
OOYOO... Mizuka!
Mizuka! Ndo mambo ya Chadema hayo. Mimi msela leo Mbunge siyo. Nipe wepa! Usipime!
Usipime!
Leo hii sitakuwa
na maneno mengi kama mnavyonijua mwanenu, nikisimama saa moja, moja na nusu
tunachama nondo, na hii ni experience toka majukwaa ya Hip Hop.
Kushinda kesi
Tunasimama
sana na nawapa hongera sana kwa sababu kesi waliyotufungulia CCM na Shitambala
kupinga ushindi imetupiliwa mbali na Jaji wa Mahakama Kuu.
Hapa sasa
wanangu tunasubiri hela ya fidia kutoka kwa CCM kwa sababu hatujafanya party
toka tushinde siyo.
Kwa hiyo sasa
tunasubiri hela ya fidia kutoka kwa CCM kwa sababu Makamba ndo aliwaambia
wafungue zile kesi na sasa Makamba hayupo kwenye game hivyo tutaenda kuchukua
mashamba yao waliyosema wanayo tufanye party tulewe siyo.
Shitambala kuondoka Chadema
Kitu cha pili
napenda niwapongeze kuondoka Shitambala ndani ya Chadema. Tumelitua zigo la
mavi ndugu zangu tumelitua... Niko Dodoma nawawakilisheni kwa mujibu wa mlivonituma.
Wakati wa mapumziko nilikuwa nasoma gazeti Shitambala anasema katumia hela
nyingi sana kuijenga Chadema Mbeya.
Katumia milioni
200 kwa ushindi wa mimi na Silinde. Siye hatujatumia hela, miye haijafika hata milioni
10 uchaguzi wangu, aache fiksi siyo.
Na zaidi yeye
ndo alikuwa anapiga mzinga kwangu mimi siyo. Kila siku anapiga simu ooh eeh
bwana kamanda una laki mbili hapo tuje tuongee kwa sababu kesho mkutano, nitakuwa
sifanyi mkutano.
Nikamcheki
nikaona huyu fiksi kwa sababu alichakachua uchaguzi uliopita, anataka
achakachue na huu, na akachakachua kweli kwa sababu masela tuna machale siyo.
Matokeo yake
ndugu yangu Shitambala ameenda kulivaa gamba ambalo wenzake wamelivua, ni
lazima limuozee hilo hilo gamba siyo. Kwa sababu kuvua gamba nako siyo dili,
tatizo la nyoka siyo gamba bali tatizo ni sumu iliyomo ndani yake.
Tutawanyonya
damu yenye sumu na kuwakata ndimi zenye sumu, tutawatoa miba na kila kitu
wakati tunaendelea kulisongesha kuelekea mwaka 2015 kwa kishindo zaidi.
CCM waache
fiksi, wache kamba wanaanza wanatajana ooh fulani fisadi, sijui tunataka
kusafisha, lakini ninashukuru kwamba wao wenyewe wamekiri kuwa ndani ya CCM
kuna mafisadi na wametuwekea majina na majina hayo ni kanjanja kwani tunajua
wako zaidi ya waliotajwa.
Mafisadi na shaka ya Urais wa Prof. Mwandosya 2015
Tunajua
Ridhiwan Kikwete ni kamba mwizi, Rostam Aziz mwizi, tunajua Lowassa mwizi,
Januari Makamba mwizi na ndiyo maana nachelea kuelewa usomi wa Prof. Mark
Mwandosya.
Kwa sababu
anataka kututumia sisi kuwapotosha watu. Wewe Prof. Mark Mwandosya na usomi
wako wote huo unashindwa kujua kuwa CCM inakufa mpaka unajiandaa kuwa Rais
kupitia CCM?
Ameshindwa
kwa usomi wake wote kuelewa kwamba CCM inakufa na hapa ndipo ninapochelea kuona
hawa wasomi sijui maprofesa, madaktari sijui manani wanakuja wanaacha taaluma
na vyuo, wanafunzi wanaandamana wao wapo tu kuchakachua tu kwenye siasa.
Kule kwao
anasema zimetumika milioni 700 mradi wa maji wakati zimetumika milioni 35
halafu anabaki anasema “Mimi ndiyo Rais nitakayewakilisha Nyanda za Juu Kusini”.
Hakuna kitu kama hicho Mwandosya.
Mwandosya
siyo tena mtoto wa dhahabu wa Mbeya. Watoto wa dhahabu mkoani Mbeya tupo hao,
wawili mimi Sugu na mwanangu Silinde pale tumefunga. Wengine watoto wa dhahabu
kutoka Mbeya tutawaletea mwaka 2015 jimbo la Rungwe Mashariki, Magharibi,
Chunya na majimbo yote tisa yaliyobaki ili tuendelee kuisukuma Mbeya yetu
jamani.
Opereshini Piga Mawe
Ndugu zangu,
sisi hatudanganyiki tena. Ndugu zangu, mimi nasema hivi, najua masela wangu wa
Sido mko hapa kwa wingi sana wa Uyole mpo hapa kwa wingi sana, nasema hivi
tumechoka. Imefikia mwisho kuuana wenyewe kwa wenyewe. Tunaibiana simu, cheni
tunapigana kibiriti, tunakufa bila kuangalia ni sababu gani vijana wanajiingiza
wizi wa simu.
Ni kwa sababu
ya maisha magumu waliyonayo toka kwa mafisadi ndiyo maana tunaishia kuwa wezi.
Hawatupi elimu, sasa mimi nasema hivi, sisi tupo wengi wao wapo wachache.
Kuanzia leo
ndani ya Jiji la Mbeya na nchi nzima natangaza ‘Operesheni Piga Mawe’. Tusipigane
mawe tena sisi kwa sisi maskini tunauana wakati tatizo tunalijua. Akipita
Ridhiwan Kikwete fisadi, piga mawe!… Akipita Lawassa fisadi, piga mawe!… Akipita
Januari Makamba fisadi, piga mawe!
Na hii si wao
tu, bali na wote wanaowasaidia. Kwa sababu siku zote tunasema anayemsaidia
gaidi naye ni gaidi. Kwa hiyo hii ni kwa wasanii wote wanaoisaidia CCM, piga
mawe na kutoingia kwenye shoo zao wanapokuja kwenye maeneo yetu.
Nyosha mikono
ili tukubaliane kwa pamoja siyo na tunakokwenda. Hata vyombo vya habari
vinavyotumika kama jukwaa la CCM navyo tunavipiga mawe kwa namna ya
kutovisikiliza….piga mawe, piga mawe, piga mawe!! - MWISHO WA HOTUBA YAKE.
OPERESHENI
GIANT NDOSYA NA TWANGA KOTEKOTE
Mbali ya ‘Operesheni
Piga Mawe’, lakini Sugu na makada wengine wa Chadema mkoani Mbeya walianzisha
operesheni ya ‘Giant Ndosya’ kwa dhamira kuu ya kumpinga Profesa Mwandosya na
kuhakikisha harudi tena jimboni mwaka 2015 huku wakiendelea na ‘Operesheni ya
Twanga Kotekote’.
Sugu
alimtaka Profesa Mwandosya kutumia muda wake wa uongozi uliosalia kwa ajili ya
kujiandaa na kustaafu kwa kuwa ndoto zake za kutaka urais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania haziwezi kutimia huku akisema ni vigumu tena kwake
kuendelea kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Rungwe Mashariki.
Sugu
aliyasema hayo wakati akihutubia wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa
‘Chadema Twanga Kotekote’ ulofanyika katika Kijiji cha Kandete, eneo la
Mwakaleli, Jimbo la Rungwe Mashariki ambalo lilikuwa linashikiliwa na Prof. Mwandosya.
Mkutano
huo ulikuwa moja ya mikutano mingi iliyoendelea kufanyika katika jimbo hilo, ikiwa
na jina la ‘Operesheni Giant Ndosya’, kama maanndalizi ya kumng’oa Prof.
Mwandosya katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015.
Sugu alisema
Prof. Mwandosya hajalitendea haki jimbo lake kwa kuwa wananchi hao wamempa
ridhaa ya kuwaongoza kwa zaidi ya miaka 15, tena akiwa na wadhifa mkubwa
serikalini, lakini kwa muda wote huo ameshindwa kuwajengea wananchi wake
barabara kuanzia Katumba hadi Mwakaleli yenye urefu wa kilometa 30 tu.
“Hata kama
Prof. Mwandosya akichaguliwa kuwa rais hatawakumbuka wananchi wa Rungwe na
badala yake atafanyia sherehe za kujipongeza Dar es Salaam, kwa kuwa huku kwao
hakuna barabara alizojenga anazoweza kupitisha magari ya Ikulu,” alisema Sugu.
Aidha,
Sugu alisema anamshangaa Prof. Mandosya kutotumia elimu kubwa aliyonayo kusoma
alama za nyakati na kuendeleza fikra za kutaka urais akiwa ndani ya Chama Cha
Mapinduzi (CCM), ambacho Sugu alidai kuwa kulikuwa na kila dalili kwamba
kufikia mwaka 2015 chama hicho kisingeweza kuwepo.
“Nawaomba
siku akija hapa mpeni ujumbe huu kuwa ajiandae kustaafu kwa kuwa hakuna urais
wala ubunge tena kwake, namshauri arudi kufundisha darasani kwa kuwa hilo ndilo
bado tunalihitaji kutoka kwake,” alisema Sugu huku akishangiliwa.
Comments
Post a Comment