- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
ZILIKUWA ni dola mia
tatu rahisi zaidi ambazo Nelson Ryan ameweza kuzipata, lakini ghafla akagundua
kwamba alikuwa amejiingiza mtegoni. Mwito wa simu, ukionekana hauna kasoro
yoyote, ulimwongoza kwenye mauaji ya binti wa Kichina aliyepiga simu huku
akiongea sana. Simu hiyo pia ikamwongoza moja kwa moja kwenye maisha ya
kihalifu ya Hong Kong. Tangu sasa na kuendelea, Ryan hakuweza kufanya chochote mpaka
atakapompata muuaji ambaye amemwingiza kwenye majanga. ENDELEA…
Akawasha sigara yake na kupuliza
moshi wote kwangu.
“Sijui: unaweza. Unaweza kujaribu
kujiosha, ukijidanganya kwamba umetengeneza ushahidi wa kutosha,” alisema,
lakini hakukuwa na mashtaka yoyote kwenye sauti yake.
“Kama ningekuwa nimeumuua,” nikaendelea,
“Ningeweza kujua muda aliokufa. Nisingeweza kuwaeleza ushahidi wangu mpaka saa
mbili na nusu, lazima ningekuwa nimeutengeneza mpaka saa tisa alfajiri.”
Alizunguka kwenye kiti change wakati
kile alichotumia kama ubongo wake kikiyumba kwa nguvu.
“Alikuwa anafanya nini ofisini kwako
majira hayo ya alfajiri?”
“Unataka nikisie?”
“Tazama, Ryan, hatujawahi kuwa na
kesi ya mauaji katika jiji hili kwa miaka mitano. Lazima niwe na habari
nitakayowapa waandishi. Mawazo yoyote uliyonayo, nitayasikiliza. Utusaidie,
nitakusaidia. Ninaweza kukukamata na kukusweka ndani kwa ushahidi nilioupata
dhidi yako, lakini ninakupa nafasi ya kunithibitisha kwamba mimi siko sahihi.
Endelea kukisia.”
“Chukulia kwa mfano alikuwa anatoka
San Francisco na siyo hapa? Pengine alitaka kuzungumza name kwa dharura?
Usiniulize kwanini au kwa nini hakuweza kumtafuta mpelelezi wa kujitegemea huko
San Francisco: pengine tu hili limetokea. Huenda alidanganya hata ndege na
kuamua kuja hapa ili aongee name na pengine alifikia uamuzi huo majira ya saa
moja usiku.
Anaweza kuwa alijua kwamba
asingeweza kufika hapa kabla ya mimi kuondoka hivyo alipiga simu. Hardwick, akiwa
tayari amenifukuza, alikuwa anasubiri hapa ili apokee simu hiyo. Alimweleza
kwamba alikuwa anakuja kwa ndege na angewasili saa tisa alfajiri. Pengine
alimwambia hakuna tatizo na yeye akamsubiri hadi alipowasili. Alipowasili
uwanja wa ndege akachukua teksi na kuja hapa. Hardwick akamsikiliza alichotaka
kuzungumza, kisha akampiga risasi.”
“Akitumia bastola yako?”
“Akitumia bastola yangu.”
“Mlango wa jengo hili unafungwa saa
tatu. Kufuli halijachezewa. Hardwick na mwanamke huyo wameingiaje hapa?”
“Hardwick atakuwa aliwasili mara tu
baada ya mimi kuondoka na kabla mlinzi hajafunga mlango wa jengo. Alijua
nilikuwa nje ya njia yake hivyo angeweza kuketi hapa na kusubiri simu. Wakati
alipowasili hapa, akaenda chini kumpokea na kumwingiza ndani. Kitasa ni cha
aina ya Yale. Hakuna ugumu wowote kukifungua ukiwa ndani.”
“Unastahili kuandika miongozo ya
filamu,” alisema kwa jeuri. “Unadhani huu ndio upuuzi utakaokwenda kuieleza
mahakama?”
“Ni vyema kuchunguza. Ni rahisi
kwake kuonekana uwanja wa ndege. Madereva wa teksi kule wanaweza kumkumbuka.”
“Chukulia kwamfano ndivyo
ilivyotokea kama unavyosema lakini badala ya huyu Hardwick unayemsema, alikuwa
ni wewe uliyemwambia kwamba unamsubiri?”
“Siyo kwamba hafahamiki. Kama
utawauliza watu wa Express Messenger Service utakuta kwamba alinitumia dola mia
tatu. Unaweza kuchunguza kwamba nilikuwa nje ya mtaa wa 33 Connaught Boulevard tangu
saa moja na nusu hadi saa tatu. Baada ya muda huo, japokuwa nilikuwepo, ni gari
moja tu iliyopita majira ya saa nane usiku, lakini sijui kama dereva aliniona
au la. Saa kumi na mbili msambaza maziwa atakwambia nilikuwa bado niko pale
pale.”
“Nina shauku tu ya kujua ulikuwa
wapi kati ya saa saba hadi saa kumi alfajiri.”
“Nilikuwa nje ya nyumba namba 33 Connaught
Boulevard.” Akapandisha mabega yake.
“Ili kuweka rekodi vizuri, leta
nione una nini kwenye mifuko yako.”
Nikatoa kila kitu kilichokuwemo
kwenye mifuko yangu na kukiweka kwenye meza. Alitazama bila kuvutiwa navyo.
“Kama ningekuwa nimeiba chochote kwake,”
nikasema, “Nisingekuwa nimekiweka mfukoni mwangu.”
Akainuka.
“Usiondoke mjini. Ninahitaji upepo
tu kidogo ili nikutupe ndani kama shahidi, hivyo chunga sana.”
Akatoka nje ya ofisi yangu, kupitia
chumba cha nje na kutokomea. Akaiacha milango yote wazi.
Nikakusanya vitu vyangu na
kuvirejesha mifukoni, halafu nikaufunga mlango na kuketi mezani na kuwasha
siagara. Mpaka sasa hawakuwa na kesi yoyote dhidi yangu, lakini walikuwa na
kitu fulani. Yote ilitegemea na nini ambacho wangekipata ndani ya saa chache
zijazo.
Japokuwa Retnick alikuwa na ubongo
wa ndege, nilikuwa na hisia kwamba muuaji alikuwa ananiwekea mtego kwa mauaji
hayo na angeweza kuweka ishara nyingine mbele ya Retnick ili nitiwe hatiani.
Kutoweka kwa bastola yangu kunaweza kumaanisha kwamba muuaji aliitumia kuua na
ingeweza kuonekana mahali ambako Retnick angeiona kwa urahisi.
Nikatoka mezani. Huu haukuwa wakati
wa kuketi nikizungusha kichwa. Nilikuwa na kazi ya kuifanya.
Nilifunga ofisi na kuelekea kwenye
lifti. Kupitia mlango wa vioo wa Jay Wayde, nilikiona kivuli cha Retnick. Alikuwa
akizungumza na Wayde, akikusanya ushahidi dhidi yangu.
Nikiwa na hisia za dharura, nikakwea
lifti hadi chini, nikawapita polisi wawili mlangoni, halafu nikavuta mtaa hadi
nilipoegesha gari langu.
Niliingia na kuufunga mlango.
Nilikuwa nimechanganyikiwa. Nilikuwa
na hamu ya ghafla ya whisky. Kunywa kabla ya saa kumi na mbili haukuwa
utaratibu wangu wa kawaida, lakini hii ilikuwa maalum. Wakati nikifungua mahali
nilipoweka chupa ya whisky, mapigo ya moyo wangu yalisimama ghafla na mdomo
ukakauka.
Kwenye droo kulikuwa na bastla yangu
.38 police special na mkoba wenye ngozi ya mjusi.
Nilikaa nikivitazama, nikihisi uti
wa mgongo umegoma kufanya kazi. Kwa kadiri nilivyokuwa ninapumua, mkoba huu
ulikuwa wa mwanamke Mchina aliyeuawa.
Itaendelea
kesho…
Comments
Post a Comment