- Get link
- Other Apps
Featured Post
Posted by
Maendeleo Vijijini
on
- Get link
- Other Apps
Na Daniel Mbega
Jana, Desemba 3, 2016 Jeshi la Polisi Kanda
Maalum ya Dar es Salaam lilisimamia wakati kampuni ya udalali ya Yono Auction
Mart ikizihamisha kwa nguvu kampuni zinazomilikiwa na mfanyabiashara Yusuf
Manji katika jengo la Quality Plaza, Kitalu Na. 189/2 Barabara ya Nyerere
jijini Dar es Salaam baada ya kampuni hizo kushindwa kulipa malimbikizo ya kodi
ya pango yanayofikia Shs. 13 bilioni.
Uamuzi wa kuzihamisha kwa nguvu kampuni
hizo kutoka kwenye jengo hilo mali ya Mfuko wa Pesheni wa Watumishi wa Umma –
PSPF ulikuja baada ya wahusika kushindwa kuhama kwa hiari kama walivyotakiwa
baada ya kupewa saa 24 na wamiliki wake.
Kampuni zilizohamishwa hapo, ambazo
zinamilikiwa na mfanyabiashara Manji – japo amejitoa kwenye uenyekiti Julai 15,
2016 ni Quality Group Company Limited, Gaming Management Limited, Q-Consult
Limited, Quality Logistics Company Limited, na International Transit Investment
Limited.
Barua ya Mkurugenzi Mtendaji wa PSPF, Adam H.
Mayingu, ya Desemba 2, 2016 kwenda kwa Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es
Salaam inaeleza kwamba kesi ilikwishaamuliwa na wahusika wanatakiwa kuhama mara
moja.
"Tunakuandikia kukueleza kuwa PSPF kama wamiliki wa jengo na
wamiliki wa hati tumemteua YONO AUCTION MART AND CO. LTD kumhamisha Quality
Group Limited kutoka kwenye jengo hilo Desemba 4, 2016. Tunaomba msaada wako
katika zoezi la kumhamisha," ilisema barua hiyo.
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kampuni ya Yono, Scholastika Kevela ambao ndio watekelezaji wa kazi
hiyo alisema, walitoa notisi ya saa 24 waliyoibandika juzi kwenye ofisi hiyo
wakiwataka waondoke wenyewe kabla ya amri hiyo halali ya Mahakama haijaisha
ifikapo leo asubuhi.
“Quality
Group na wenzake wanne wanatakiwa kuondoka na sisi leo(jana) tumekuja kuwaondoa
na ndio unaona wanapakia vitu vyao na kuondoka, wanadaiwa Dola Milioni 601 sawa
na Sh Bilioni 13, ambazo kila mara akiambiwa alipe amekuwa akikimbilia mahakamani
zaidi ya miaka 10 sasa”,alisema Kevela.
Alisema
Mfuko wa PSPF,unaidai Kampuni ya Quality Group fedha hizo za upangaji, lakini
kila anapotakiwa kulipa amekuwa akigoma na kukimbilia mahakamani kuweka
pingamizi la kulipa ili aendelee kukaa bure na kwamba uamuzi wa Mahakama Kuu
uliotolewa Novemba 24, umemtaka aondoke ndani ya saa 24 na kulipa deni
analodaiwa.
“Tulikuja
kubandika tangazo la hukumu hiyo la kumtaka aondoke mwenyewe kwenye jengo hilo
lakini akawa anachana na watu wake na sisi tukaongeza watu wetu kulinda na sasa
ameanza kutoa mali zake na hadi kesho anapaswa awe amemamliza,”alisema Kevela.
Alisema
pamoja na kutoa vitu vyake ndani ya jengo hilo amepewa muda wa siku 14 kisheria
awe amelipa deni hilo na kama atashindwa kulipa mali zake zitakamatwa na kuuzwa
ili kupata fedha za kulipa deni analodaiwa na PSPF.
Novemba 24, 2016 Mahakama Kuu Kitengo cha
Ardhi, mbele ya Jaji J. S. MGETTA, ilitoa hukumu ya kesi nne ambazo
ziliwahusisha walalamikaji na walalamikiwa wale wale katika eneo moja, ambapo
pamoja na mambo mengine, ilitupilia mbali madai yote ya walalamikaji katika
kesi tatu na kuyatupa madai mengine katika kesi ya nne.
Walalamikaji katika kesi hizo nne walitaka
walipwe fidia ya jumla ya Dola 38,847009.58 pamoja na Shs. 900,000,000, lakini
baada ya kuyatupa madai hayo, mbali ya kukubali walalamikaji walipwe Shs.
100,000,000 tu na kila upande kubeba gharama za kesi, Mahakama iliagiza walalamikaji
hao waondoke mara moja kwenye jengo la Quality Plaza, sasa PSPF Plaza, mali ya
Mfuko wa Pensheni wa Watumishi wa Umma – PSPF.
Kesi hizo za ardhi Na. 33/2009, Na.
40/2011, Na. 59 ya 2012, na Na. 77/2012 zilihusisha kampuni tano zilizo chini
ya mfanyabiashara Yusuf Manji – japo ametangaza kujitoa kwenye uenyekiti na
kubakia kuwa mshauri – ambazo ni Quality Group Company Limited, Gaming
Management Limited, Q-Consult Limited, Quality Logistics Company Limited, na
International Transit Investment Limited ambazo zilikuwa walalamikaji kwa
upande mmoja, dhidi ya walalamikiwa Image Properties and Estate Limited, Quality
Plaza Limited, Yohana H. Malundo ambaye ni Mfilisi wa Quality Plaza Limited na
Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa Watumishi wa Umma – PSPF.
Katika Shauri la Ardhi Na. 33 la 2009,
walalamikaji Namba 1 na Namba 3 - Quality Group Company Limited na Quality
Logistics Company Limited - walikuwa wanaiomba mahakama imwamuru mshtakiwa
namba moja Image Properties and Estate Limited awalipe jumla ya Dola za
Marekani 1,508,324.16 kutokana na kuvunja mkataba na usumbufu, lakini pia fedha
hizo ziongezwe na riba ya asilimia 21 ya kiwango cha sasa cha ubadilishaji
fedha.
Katika Shauri la Ardhi Na. 40 la mwaka
2011, walalamikaji Quality Group Company Limited na Q-Consult Limited walikuwa
wanaomba walipwe na mshtakiwa Namba 2 Quality Plaza Limited jumla ya Dola
3,000,000 za fidia na kuvunjwa kwa mkataba.
Aidha, katika Shauri la Ardhi Na. 59 la
mwaka 2012, mlalamikaji wa kwanza Quality Group Company Limited alikuwa
anaiomba Mahakama imwamuru mshtakiwa Namba 1 Image Properties and Estate
Limited pamoja na mambo mengine amlipe jumla ya Shs. 900,000,000 kutokana na
usumbufu na hasara.
Kwenye Shauri la Ardhi Na. 77 la mwaka
2012, walalamikaji namba 1, 2 na 4 - yaani Quality Group Company Limited,
Gaming Management Limited na Quality Logistics Company Limited pamoja na mambo
mengine, walikuwa wanaiomba Mahakama kuwaamuru washtakiwa wote wanne - Image
Properties and Estate Limited, Quality Plaza Limited, Yohana H. Malundo ambaye
ni Mfilisi wa Quality Plaza Limited na Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya
Jamii wa Watumishi wa Umma - PSPF - jumla ya Dola 34,338,685.42 kutokana na
usumbufu pamoja na mambo mengine.
Katika mashauri hayo yote, walalamikaji
waliwakilishwa na wakili msomi Arwa Yusufu wakati walalamikiwa waliwakilishwa
na Benitho Mandele, Rwehumbiza, Mweletwa na Chaula, mbele ya Jaji J.S. Mgetta.
Katika hukumu yake, ambayo ilisainiwa na
Mhe. F.H. Mahimbali, Naibu Msajili wa mahakama hiyo, Mahakama iliyatupilia
mbali madai ya fidia yote katika kesi tatu Na. 33/2009, Na. 40/2011 na Na.
77/2012 yanayofikia jumla ya Dola 38,847009.58 na Shs. 900,000,000 ambayo
yameshindwa kuthibitishwa uhalali wake.
Hata hivyo, Mahakama hiyo imekubaliana na
sehemu ya madai ya fidia katika Shauri Na. 59 la 2012 na kuamuru kwamba
Mshtakiwa wa Kwanza ama Mshtakiwa wa Pili amlipe mlalamikaji Namba 1 kiasi cha
Shs. 100,000,000 kama fidia ya hasara huku kila upande ukibeba gharama za
uendeshaji wa kesi.
Aidha, Mahakama imeagiza kwamba
walalamikaji wote wanatakiwa kuondoka mara moja kwenye jengo husika kwa sababu
wamekiuka agano kuu la kulipa kodi na gharama mbalimbali na kuagiza kwamba, kwa
vile walalamikiwa walikuwa hawajawasilisha kiasi halisi ambacho walalamikaji
wanadaiwa kama kodi, basi pande hizo mbili zikakokotoe hesabu kamili na
wahusika walipe.
Itakumbukwa kwamba, Desemba 22, 2010,
gazeti la Tanzania Daima liliwahi kuripoti kwamba mfanyabiashara maarufu nchini
Yusuf Manji alikuwa amepewa Notisi ya saa 48 na Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi
wa Umma (PSPF), kuhama katika jengo la Quality Plaza Complex lililoko Kitalu
Na. 189/2 Barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam ambalo ni mali ya PSPF na
Manji ni mpangaji anadaiwa kukiuka masharti ya mkataba wa upangishwaji kwa
kushindwa kulipa kodi.
Wakili wa PSPF, Benitho Mandele, alisema
katika barua yake yenye kumbukumbu namba DLA/IMAGE/2010/12 kwenda kwa
Mkurugenzi Mkuu wa Quality Group Limited, Manji alikuwa anadaiwa kodi ya
kuanzia Aprili, 2009 hadi Desemba 2010, hivyo jumla ya deni lote lilikuwa Dola
2,335,189.06 za Marekani. Barua hiyo ya Notisi ilikwenda kwenda kwa Mkurugenzi wa Quality Group
Limited, Gaming Management Limited, Quality Ligistics Co. Limited,
International Transit Ivestment Limited na Q-Consult Limited, ambapo Manji
alipewa nakala ya barua hiyo kama Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Quality
Group Limited.
Lakini taarifa zinaeleza kwamba, Manji
ndiye aliyewauzia PSPF jengo hilo kwa gharama ya Shs. 36 bilioni ikiwa ni
thamani iliyo mara 10 ya bei halisi.
Jambo la kusikitisha ni kwamba, PSPF
hawakuwa na hati ya ardhi ya jengo hilo la Quality Plaza. Ushahidi wa maelezo
ni huu hapa wa habari ambazo ziliwahi kuripotiwa na magazeti;
Despite paying billions,
PSPF doesn`t fully own Quality Plaza
THISDAY REPORTER
Dar es Salaam
THE Public Service Pensions Fund does not own the land where
Quality Plaza is located despite paying a staggering 36bn/- for the property,
THISDAY can now reveal.
Instead, the pensions fund was given only partial ownership of
some of the sub-titles tied up to the property located along Nyerere Road in
Dar es Salaam. Our investigations have revealed that the Quality Plaza building
has a total of 11 certificates of title.
The titles are for separate parts of the ground floor,
mezzanine, first and second floors only.
In a highly unusual move, PSPF agreed to pay through the nose
for the building, only to end up with nine of the 11 sub-titles for the
property and two of the sub-titles to the building belong to a ‘mystery’ owner.
This means that despite paying a staggering 36bn/- for the
two-storey Quality Plaza, PSPF does not own the main title. Furthermore, the
pensions fund does not also own some parts of the building.
Under the share purchase agreement, PSPF agreed to partial
ownership of the building although it paid a staggering amount for the
property.
"The building on Plot No.
189/2, Nyerere Road, Dar es Salaam is subdivided into 11 ‘Certificates of
Title(s)’ of which 2 are not owned by the vendors and which therefore are
acknowledged by both -- the vendors and the purchaser -- that they do not form
part of this agreement nor represented as that which is here-in referred to as
the property," says the share purchase
agreement.
The agreement was signed on November 19, 2004, by the PSPF
Director-General, Ms Hawa Mmanga, and the pensions fund legal officer, Mr Ngabo
Patrick Ibrahim. The Chief Executive Officer of Quality Group Limited, Yusuf
Manji, and the company?s director for corporate affairs, Rakesh Mehta,
represented the sellers.
The pensions fund paid a total of 36bn/- for the purchase of 100
per cent of the shares in a company known as ‘Quality Plaza Limited’, which
owns the sub-titles to the property. Surprisingly, instead of buying just the
property alone, PSPF bought an entire company, which means that it risks
covering all outstanding taxation liabilities for the company.
If the Tanzania Revenue Authority (TRA) carries out a new
assessment on previous tax liabilities for Quality Plaza Limited, PSPF would
have to meet these costs.
The pensions fund is also liable to pay the terminal benefits of
employees of the private company that it has taken over.
The deal, which has been described as ‘a disaster’ by financial
experts, implies that the PSPF has now walked into unknown liabilities. Our
investigations revealed that the former owners of Quality Plaza Limited pushed
up the value of their company from 30bn/- to 36bn/- just a few days before the
sale was made.
Prior to the deal, shareholders of Quality Plaza Limited were
listed as Quality Group Limited (95 per cent) and Mr Mehboob Manji (5 per
cent).
Our investigations show that Quality Plaza Limited filed a
notice of increase in the nominal capital to 36bn/- on November 10, 2004. A few
days later, PSPF hurriedly bought the company for the exact 36bn/- in a cobbled
up transaction.
Sources close to the deal say the pensions fund was in a hurry
to conclude the deal -- it ordered valuation to be done within just one week
and signed the share purchase agreement just a week after receiving the
valuation report.
Source: THISDAY archives,
2006
Now Manji prays for out
of court settlement
By Edwin Agola
25th December 2010
Quality Group director Yusuf Manji has asked Temeke Land
tribunal in Dar es Salaam to suspend hearing of a chamber application against
Image Properties that was lined up for hearing yesterday and now prefers
amicable settlement out of court.
Manji's counsel, Joseph Thadayo, appearing for Quality Group,
told tribunal chairman Mlyambina Kaare in the city that his client had promised
to settle rent accruals totalling 5bn/- by January 31, 2011.
But advocate Benitho Mandele from Destiny Law Attorneys for
Image Properties, when reached for comment, said he had written a letter
seeking clarification on the mode of payment.
"I have written a letter to Yusuf Manji asking to be told
how the debt would be sorted out, and if by January 8 there will be no
response, we have instructed Majembe Auction Mart to execute the 48-hour notice
to forcibly evict Manji from Quality Plaza premises without further
notice," said Mandele.
Quality Group had filed a chamber application with the tribunal
asking it to jail Image Properties managing director for contempt of court.
Image Properties, through its lawyer Mandele, filed a counter
affidavit seeking legal redress because the said chamber application was marred
with incurable irregularities, following which the tribunal on Monday, struck
out part of the application, which was set for hearing yesterday.
On November 19, 2004 Manji sold Quality Plaza located along
Nyerere road to the Public Service Pension Fund (PSPF) for 36bn/-, according to
sales documents availed to The Guardian, but decided to occupy one-third of the
building on the understanding that he would pay a monthly rent of 300m/-, which
he has failed to honour, to date.
The property was acquired using the fund members' contributions
and now the pensioners cannot be paid their dues due to this debt, according to
Mandele.
On Monday PSPF slapped Manji with a 48-hour notice to vacate the
Quality Plaza complex for failure to pay 3.5bn/- in unpaid rent covering the
period from April 2009 to date, following which he now seeks to settle the
matter out of court.
SOURCE: THE GUARDIAN
Aidha, ikumbukwe pia kwamba, mnamo Juni 4,
2012, Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Umma - PSPF, ulimtaka kwa mara nyingine
mfanyabiashara Yusuf Manji kuhama mara moja katika jengo la Quality Plaza.
Wakati huo Manji alikuwa anadaiwa na PSPF karibu Shs. bilioni 5, ambazo ni
malimbikizo ya kodi ya pango.
Kwa muda mrefu Manji alikuwa akitajwa
kufanya biashara zenye utata na mifuko ya hifadhi za jamii na alifanikiwa
kuiuzia PSPF jengo la Quality Plaza na Mufuko wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) kuiuzua
maghala ya Urafiki - Ubungo kwa Shs. 46 bilioni ambayo aliyajenga kwa mkopo wa
Shs. 9 bilioni kutoka mfuko huo huo.
Uamuzi wa PSPF kumhamisha Manji wakati huo ulifikiwa
Ijumaa ya Aprili 1, 2011 baada ya mfuko huo kubanwa na Wabunge wa Kamati Hesabu
za Mashirika ya Umma (POAC), iliyokuwa ikiongozwa na aliyekuwa Mbunge wa Kigoma
Kaskazini (Chadema), Zitto Kabwe.
Katika barua ya PSPF kwenda kwa kampuni ya
Image Properties & Estate inayosimamia uendeshaji wa Quality Plaza, mfuko
huo uliitaka kampuni ya Quality Group Limited kuondoka mara moja katika jengo
hilo vinginevyo hatua kali za kisheria zingechukuliwa. Muda mfupi nyuma,
Quality Group Limited ilikuwa imeiomba Mahakama kuzuia kuondolewa kwao katika
jengo hilo, maombi ambayo muda wake ulishakwisha lakini PSPF wakawa wanachelewa
kuchukua hatua huku taasisi hiyo ikiwa na hali mbaya ya kifedha kiasi cha
serikali kuombwa na POAC kuinusuru kwa kuwekeza zaidi.
Makampuni mengine ya Manji yaliyomo katika
jengo hilo ni pamoja na kampuni aliyoichukua kwa Chama cha Mapinduzi (CCM)
katika mazingira tata ya Gaming Management Limited, Quality Ligistics Co.
Limited, International Transit Ivestment Limited na Q-Consult Limited.
HII NDIYO NOTISI ALIYOPEWA KUHAMA KWA HIARI
HII NI BARUA KWENDA KWA RPC WA DAR
HII NI HUKUMU YA KESI
Comments
Post a Comment