Featured Post

SUNGURA ALIYETUNZWA VIZURI ANAZAA MARA NNE KWA MWAKA WATOTO 40!



 Sungura mwenye afya bora huzaa watoto wengi

 Watoto wadogo wa sungura baada ya kuzaliwa.

 

Na Daniel Mbega

IKIWA tayari umekwishaanzisha ufugaji wa sungura, mambo ya msingi kuzingatia kwanza ni kuangalia tabia zao kwa sababu zinatofautiana kutoka eneo moja hadi jingine.
Kwa kawaida, sungura jike aliyeshika mimba hujulikana kwa mwenendo wake, huwa mtulivu, na hula chakula kidogo.
Baada ya siku 30 hadi 32 hujitoa manyoa yake kujenga kiota na huzaa siku chache baadaye. Sungura kwa mara moja huweza kuzaa kati ya mtoto mmoja hadi watoto 15, lakini sungura anayezaa watoto wengi ni sharti awe na afya njema la sivyo watoto hawa wanaweza kufa kwa kukosa chakula cha kutosha.
Nimeelezea katika makala zilizotangulia, kwamba katika mazingira yao ya asili porini, sungura huzaliana kila baada ya wiki nne, lakini kwa hawa wa kufuga unaweza kuwatengea kati ya wiki 5-9 na kuwapa siku 28 – 33 za kubeba mimba hadi kuzaa.
PATA MWONGOZO UTAKAOKUSAIDIA KATIKA UFUGAJI NA JINSI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI YAKIWEMO MAGONJWA.
WASILIANA NA DANIEL MBEGA KWA SIMU HII +255 656 331974 ILI UPATE NAKALA YAKO SASA KWA GHARAMA NAFUU KABISA YA SHS. 20,000/= TU!! … FUATA LINK HII UPATE MAELEZO ZAIDI.


Comments