Featured Post

HAYA NDIYO MAGONJWA MATANO HATARI YA SUNGURA


Na Daniel Mbega
SUNGURA ni wanyama wastahimilivu wa mazingira mbalimbali kiasi cha kushindwa kuugua ovyo kama ilivyo kwa wanyama wengine wa kufuga, lakini wanyama hawa ni laini, kiasi ambacho wanaweza kuwa katika hatari ya kukumbwa na magonjwa yanayochanganya, hata kama watatunzwa vizuri namna gani.

Kama ilivyo kwa hali yoyote ambayo inaweza kuwaathiri sungura wako au mnyama mwingine wa kufugwa, kulitambua tatizo mapema na kulishughulikia haraka kwa kuwatibu linaweza kuleta mabadiliko makubwa kuhusu kuishi kwa sungura wako na kupona kabisa.
Sungura siyo wanyama wanaokula nyama wala si wanyama hatari na mara nyingi wako hatarini kuliwa na wanyama wengine.
Kwa sababu ya hali hiyo, sungura pia wanaweza kupatwa na maumivu au ugonjwa, na kuonyesha dalili ambazo zinaweza kuwa ishara kwa wanyama hatari kuwashambulia. Ninazungumzia kuhusu asili yao ya kuishi porini n ahata unapowafuga.
Hii inamaanisha kwamba ni vigumu kwetu kama wafugaji wa sungura kubaini kwa urahisi wakati mambo yanapokwenda mrama, na kujifunza kuhusu baadhi ya dalili za mwanzo za tatizo kunaweza kuwa changamoto ya kujifunza kwa undani.
Yafuatayo ni baadhi ya matatizo ya msingi yanayowapata sungura ambayo yanaweza kuwa vigumu kuyatambua katika hatua za mwanzo, na jinsi ambavyo unaweza kuyagundua.
PATA MWONGOZO UTAKAOKUSAIDIA KATIKA UFUGAJI NA JINSI YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI YAKIWEMO MAGONJWA.
WASILIANA NA DANIEL MBEGA KWA SIMU HII +255 656 331974 ILI UPATE NAKALA YAKO SASA KWA GHARAMA NAFUU KABISA YA SHS. 20,000/= TU!! … FUATA LINK HII UPATE MAELEZO ZAIDI.

Comments